Hamia kwenye habari


JIFUNZE BIBLIA UKIONGOZWA NA MWALIMU

Furahia Maisha Milele!

Funzo hili la Biblia bila malipo litakusaidia kupata majibu ya maswali kama vile:

  • Ninaweza kupataje furaha maishani?

  • Je, uovu na kuteseka kutakwisha?

  • Je, nitawaona tena wapendwa wangu waliokufa?

  • Je, kweli Mungu ananijali?

  • Ninaweza kusali jinsi gani ili Mungu anisikilize?

Bila Malipo

Utapata masomo yote bila malipo kutia ndani chapisho lenye kichwa Furahia Maisha Milele! ambacho ni mwongozo wa funzo pamoja na nakala ya Biblia ikiwa unahitaji.

Litakufaa

Unaweza kukutana na mwalimu moja kwa moja au mtandaoni—wakati wowote na mahali popote.

Huwajibiki

Unaweza kuacha kujifunza wakati wowote—huwajibiki.

Funzo hili la Biblia linafanywaje?

Mwalimu wako atakusaidia kujua yale ambayo Biblia inafundisha somo baada ya somo. Kwa kujifunza Biblia ukitumia Furahia Maisha Milele!, hatua kwa hatua utajifunza ujumbe ulio katika Biblia na jinsi unavyoweza kukusaidia. Ili upate habari zaidi tazama video hii au upitie maswali yanayoulizwa mara nyingi kuhusu funzo hili.

Je, ungependa kujua yaliyomo?

Pitia masomo ya kwanza ya funzo hili.

Uko tayari kujaribu?

Bonyeza kitufe hiki ili kupanga somo lako la kwanza la Biblia la kibinafsi.