Ona video zinazopatikana

Mikutano ya Mashahidi wa Yehova

Pata habari zaidi juu ya mikutano yetu. Tafuta fasi ya mikutano karibu na kwenye unaishi.

Tafuta Adresi Karibu na Wewe (opens new window)

Mikutano Yetu Inafanywa Namna Gani?

Mashahidi wa Yehova wanakusanyika mara mbili kwa juma ili kumuabudu Mungu. (Waebrania 10:24, 25) Kwenye mikutano hiyo, ambayo kila mutu anaalikwa, tunajifunza yale ambayo Biblia inafundisha na namna tunavyoweza kutumia mafundisho ya Biblia katika maisha yetu.

Mikutano yetu mingi inatia ndani mazungumuzo pamoja na wasikilizaji, ambayo inafanana tu na mazungumuzo kati ya mwalimu na wanafunzi. Inaanza na kumalizika kwa wimbo na sala.

Iwe wewe ni Shahidi wa Yehova ao hapana, unaweza kuhuzuria mikutano yetu. Tunakaribisha kila mutu. Hakuna kulipa. Hautaombwa kutoa sadaka.