APRILI 26, 2019
KOLOMBIA
Mashahidi wa Yehova Watambuliwa kwa Kuwapa Wafungwa Elimu ya Biblia Nchini Kolombia
Kwa miaka zaidi ya 20, ndugu zetu nchini Kolombia wamekuwa wakiwafunza wafungwa Biblia bila malipo. Novemba 30, 2018, Kituo cha Elimu cha Paulo Freire kiliwapa Mashahidi wa Yehova cheti kilichoonyesha kwamba walitambua kazi yao ya kuwapa wafungwa elimu ya Biblia katika gereza moja katika jiji la Valledupar. Kwa sasa, wafungwa 50 wamejiunga na masomo hayo ya Biblia.
Kotekote nchini Kolombia, Mashahidi wa Yehova wanatoa mafunzo kama hayo katika magereza 65, ambako wanaongoza mafunzo ya Biblia 782. Jumla ya watu 60 wamefikia hatua ya ubatizo tangu mwaka wa 1996.
Néver Antonio Cavadía alianza kujifunza Biblia alipokuwa gerezani na akabatizwa mwaka wa 1998. Baadaye aliachiliwa kutoka gereza la Valledupar mwaka wa 2007. Akieleza manufaa aliyopata kwa kupata elimu hiyo, alisema hivi: “Kanuni za Biblia zilinilinda na kunisaidia kuwa na hekima inayotumika nilipokuwa gerezani. Pia, zilinichochea kufanya mabadiliko makubwa maishani na kudumisha tumaini.”
Ulimwenguni pote, jitihada zetu za kuwafikia wale walio gerezani zinapatana na mapenzi ya Yehova kwamba “watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli”—1 Timotheo 2:4.