Hamia kwenye habari

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutiwa Damu Mishipani?

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutiwa Damu Mishipani?

Jibu la Biblia

 Biblia inatuamuru tusile damu. Kwa hiyo, hatupaswi kukubali damu nzima au sehemu zake za msingi kwa njia yoyote ile, iwe tunaila kama chakula au tunatiwa mishipani. Fikiria maandiko yafuatayo:

  •   Mwanzo 9:4. Baada ya Gharika, Mungu alimruhusu Noa na familia yake kula nyama lakini akawaamuru wasile damu. Mungu alimwambia hivi Noa: “Isipokuwa tu nyama pamoja na nafsi yake—damu yake—msile.” Amri hiyo inawahusu pia wanadamu wote kuanzia wakati huo na kuendelea kwa kuwa wote ni wazao wa Noa.

  •   Mambo ya Walawi 17:14. “Hamtakula damu ya mwili wa namna yoyote, kwa sababu nafsi ya kila mwili wa namna yoyote iko katika damu yake. Mtu yeyote atakayeila atakatiliwa mbali.” Mungu aliona nafsi, au uhai, umo katika damu na ni mali yake. Ijapokuwa taifa la Israeli ndilo lililopewa sheria hiyo, inaonyesha kwamba Mungu alichukua kwa uzito sana sheria ya kutokula damu.

  •   Matendo 15:20. ‘Jiepusheni na damu.’ Mungu aliwapa Wakristo amri hiyohiyo aliyompa Noa. Historia inaonyesha kwamba Wakristo wa mapema walikataa kula damu nzima, hata ikiwa ni kwa ajili ya matibabu.

Kwa nini Mungu anatuamuru tujiepushe na damu?

 Kuna sababu nzuri za kimatibabu za kuepuka kutiwa damu mishipani. Hata hivyo, sababu muhimu zaidi ya Mungu kutuamuru tujiepushe na damu ni kwamba inawakilisha kitu kitakatifu machoni pake.—Mambo ya Walawi 17:11; Wakolosai 1:20.