Hamia kwenye habari

Ibilisi Anaishi Wapi?

Ibilisi Anaishi Wapi?

Jibu la Biblia

 Akiwa kiumbe wa roho, Ibilisi huishi katika makao yasiyoonekana. Hata hivyo, si kwenye moto wa mateso ambapo huwatesa watenda maovu, kama inavyoonyeshwa katika picha iliyo kwenye makala hii.

“Vita mbinguni”

 Kwa muda fulani, Shetani Ibilisi alikuwa na uhuru wa kutembea huku na kule katika makao yasiyoonekana ya roho, kutia ndani kusimama mbele za Mungu akiwa pamoja na malaika waaminifu. (Ayubu 1:6) Hata hivyo Biblia ilitabiri kwamba kungekuwa na “vita mbinguni” ambavyo vingesababisha Shetani “kutupwa duniani.” (Ufunuo 12:7-9, Habari Njema kwa Watu Wote) Masimulizi ya Biblia na matukio ya ulimwengu yanathibitisha kwamba vita hivyo tayari vilitokea mbinguni. Ibilisi sasa hawezi tena kurudi mbinguni.

 Je, hilo linamaanisha kwamba Ibilisi anaishi mahali fulani hususa duniani? Kwa mfano, jiji la kale la Pergamamu lilionwa kuwa “mahali kilipo kiti cha ufalme cha Shetani” na “mahali anapokaa Shetani.” (Ufunuo 2:13) Kwa kweli, huenda maneno hayo yakarejelea jinsi ambavyo ibada ya kishetani ilivyokuwa imejaa katika jiji hilo. Biblia inasema kwamba Ibilisi anatawala “falme zote za dunia inayokaliwa,” kwa hivyo hakai mahali pamoja duniani na hawezi kurudi mbinguni.​—Luka 4:​5, 6.