Hamia kwenye habari

Sifurahii Maisha Yangu—Je, Dini, Mungu, au Biblia Inaweza Kunisaidia?

Sifurahii Maisha Yangu—Je, Dini, Mungu, au Biblia Inaweza Kunisaidia?

Biblia inajibu

 Ndiyo. Biblia, kitabu cha zamani chenye hekima, ina majibu ya maswali muhimu sana kuhusu maisha na inaweza kukusaidia ujihisi vizuri na kuwa mwenye furaha. Fikiria maswali fulani ambayo inajibu.

  1.   Je, kuna Muumba? Biblia inasema kwamba Mungu ‘aliumba vitu vyote.’ (Ufunuo 4:11) Akiwa Muumba wetu, Mungu anajua mambo yanayoweza kutufanya tuwe na furaha na kuridhika katika maisha.

  2.   Je, Mungu anatujali? Badala ya kuonyesha kwamba Mungu amejitenga na wanadamu, Biblia inasema: “Hayuko mbali sana na kila mmoja wetu.” (Matendo 17:27) Mungu anajua vizuri mambo yanayokupata maishani na anataka kukusaidia ili ufanikiwe.—Isaya 48:17, 18; 1 Petro 5:7.

  3.   Kumjua Mungu kunaweza kunisaidiaje nijihisi vizuri? Mungu alituumba tukiwa na “uhitaji wa kiroho,” njaa tuliyozaliwa nayo ya kuelewa maana na kusudi la uhai. (Mathayo 5:3) Uhitaji wetu wa kiroho pia unatia ndani tamaa ya kumjua Muumba wetu na kuwa na uhusiano pamoja naye. Mungu atathamini jitihada zako za kutaka kumjua yeye, kwa kuwa Biblia inasema: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.”—Yakobo 4:8.

 Mamilioni ya watu wametambua kwamba kujenga urafiki na Mungu kumeboresha furaha yao kwa ujumla na kumewaonyesha jinsi ya kujihisi vizuri. Ingawa kumjua Mungu hakutaondoa matatizo katika maisha yako, hekima yake iliyo kwenye Biblia inaweza kukusaidia

 Dini nyingi ambazo hutumia Biblia kwa kweli hazifuati mafundisho yake. Tofauti na hilo, dini ya kweli, ambayo inakubali mambo ambayo Biblia inasema hasa, itakusaidia umjue Mungu.