Hamia kwenye habari

Kwa Nini Tusali Katika Jina la Yesu?

Kwa Nini Tusali Katika Jina la Yesu?

Jibu la Biblia

 Tunapaswa kusali kwa Mungu katika jina la Yesu kwa sababu hiyo ndiyo njia pekee ambayo Mungu ameandaa ya kumfikia. Yesu alisema: “Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu.” (Yohana 14:6) Yesu pia aliwaambia hivi mitume wake waaminifu: “Kwa kweli kabisa ninawaambia, Mkimwomba Baba jambo lolote atawapa katika jina langu.”—Yohana 16:23.

Sababu zaidi kwa nini tusali katika jina la Yesu

  •   Tunamheshimu Yesu na Baba yake, Yehova Mungu.—Wafilipi 2:9-11.

  •   Tunaonyesha kwamba tunathamini kifo cha Yesu kuwa uandalizi ambao Mungu amefanya ili tupate wokovu.—Mathayo 20:28; Matendo 4:12.

  •   Tunatambua daraka la Yesu akiwa Mpatanishi, au Mwombezi, kati ya Mungu na wanadamu.—Waebrania 7:25.

  •   Tunaheshimu huduma ya Yesu akiwa Kuhani Mkuu ambaye anaweza kutusaidia kuwa na uhusiano mzuri na Mungu.—Waebrania 4:14-16.