Hamia kwenye habari

Ramani za Biblia

Ramani za Biblia

Broshua“Ona Nchi Nzuri” ni kijitabu kilicho na Ramani za Biblia zinazoonyesha maeneo hususa yaliyotajwa katika Biblia na kinaweza kukusaidia kuboresha funzo lako la kibinafsi. Biblia inataja sehemu mbalimbali, majiji na nchi nyingi. Kwa kutumia ramani hizi unaweza kufurahia usomaji wako wa Biblia na kufanya funzo lako liwe halisi zaidi. Broshua“Ona Nchi Nzuri” itakusaidia kupata na kuwazia sehemu mbalimbali ambazo zimetajwa katika masimulizi ya Biblia. Pia itakusaidia kuelewa jinsi jiografia ya nchi ilivyochangia katika matukio mbalimbali ya Biblia.

Broshua“Ona Nchi Nzuri” ina ramani nyingi zenye rangi na chati zinazoonyesha maeneo mbalimbali yanayotajwa katika Biblia. Broshua hii ina picha, michoro ya kompyuta, na mambo mengine mengi yatakayoboresha funzo lako la kibinafsi.

Ramani hizi za Biblia zitakuwezesha

  • kuelewa safari za Abrahamu, Isaka, na Yakobo

  • kuona njia ambayo Waisraeli walipitia walipotoka Misri kwenda kwenye Nchi ya Ahadi

  • kuona mahali eneo la Israeli lilipokuwa kwa kulinganishwa na maeneo ya maadui wao

  • kuona maeneo ambayo Yesu alienda wakati wa huduma yake

  • kuelewa ukubwa wa milki zinazotajwa katika Biblia kama vile Babiloni, Ugiriki’ na Roma

Unaweza kupata kijitabu hiki kilicho na ramani za Biblia bila malipo kwa kutumia Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO.