Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

AMKENI! Na. 2 2018 | Siri 12 za Mafanikio Katika Familia

Siri 12 za Familia Ambazo Zimefanikiwa

Mara nyingi tunasikia kuhusu kile kinachosababisha familia fulani ziwe na matatizo. Hata hivyo, ni nini kinachoziwezesha familia nyingine kufaulu?

  • Kati ya mwaka 1990 na 2015, kiwango cha talaka nchini Marekani kiliongezeka mara mbili kwa wenzi wa ndoa walio na umri wa miaka zaidi ya 50 na mara tatu kwa wale walio na miaka zaidi ya 65.

  • Wazazi wako njia panda: Baadhi ya wataalamu wanapendekeza kwamba inafaa watoto wasifiwe kila wakati, ilhali wengine wanasema kwamba watoto hawapaswi kudekezwa hata kidogo.

  • Vijana wanaingia utu uzima bila kuwa na sifa wanazohitaji ili wafanikiwe maishani.

Ingawa hivyo, ukweli ni kwamba . . .

  • Inawezekana kabisa ndoa ikadumu na kuwa yenye furaha.

  • Wazazi wanaweza kujifunza kuwatia nidhamu watoto wao kwa upendo.

  • Vijana wanaweza kusitawisha sifa watakazohitaji wakiwa watu wazima.

Jinsi gani? Toleo hili la Amkeni! litazungumzia siri 12 zinazoziwezesha familia kufanikiwa.

 

1: Ushikamanifu

Mapendekezo matatu yanayoweza kuwasaidia wenzi wa ndoa wasiachane.

2: Ushirikiano

Je, unamwona mwenzi wako wa ndoa kama mtu mnayeishi naye tu chumba kimoja?

3: Heshima

Tambua maneno na matendo ambayo yatafanya mwenzi wako ahisi anaheshimiwa.

4: Kusameheana

Unaweza kufanya nini ili badala ya kukazia udhaifu wa mwenzi wako, uone sifa zake nzuri?

5: Mawasiliano

Jifunze mambo matatu yatakayokusaidia uwe karibu na watoto wako.

6: Nidhamu

Je, nidhamu hufanya mtoto asijiamini?

7: Kanuni za Maisha

Unapaswa kuwafundisha watoto wako kanuni gani?

8: Kielelezo

Ili maneno yako yaguse moyo wa mtoto wako, lazima yapatane na matendo yako.

9: Kujitambua

Vijana wanawezaje kuepuka kushinikizwa kutenda kinyume na mambo wanayoamini?

10: Uaminifu

Kuwa mwenye kuaminika machoni pa wazazi wako ni hatua muhimu ya kuingia utu uzima.

11: Bidii

Kujifunza kuwa mwenye bidii ukiwa kijana kutakusaidia ufanikiwe katika kila jambo unalofanya maishani.

12: Malengo

Kufikia malengo kutakuwezesha ujiamini zaidi, uimarishe urafiki na wengine, na kufanya uwe na furaha zaidi.

Msaada Zaidi Kwa Ajili ya Familia

Ushauri wa Biblia unaweza kukusaidia uwe na ndoa nzuri na familia yenye furaha.