Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Anzisha Urafiki na Watu Mbalimbali

Anzisha Urafiki na Watu Mbalimbali

Tatizo

Tukijitenga na watu ambao tunahisi ni tofauti na sisi, tutachochea hisia za ubaguzi. Na tukichagua marafiki ambao wana mtazamo kama wetu, huenda tukawa na maoni kwamba wengine wanapaswa kufikiri, kuhisi na kutenda kama sisi.

Kanuni ya Biblia

“Fungueni kabisa mioyo yenu.”​—2 WAKORINTHO 6:13.

Kanuni hiyo inamaanisha nini? Moyo unaweza kumaanisha hisia zetu kutia ndani upendo tulionao kuelekea watu wengine. Ikiwa watu tunaowapenda ni wale tu walio na hali, sifa na mtazamo kama wetu, tutakuwa tumefunga moyo wetu. Ili kuepuka tatizo hilo, ni lazima tuwe tayari kufanya urafiki na watu walio tofauti na sisi.

Faida za Kufanya Urafiki na Watu Mbalimbali

Tunapowajua watu kibinafsi, tunaanza kuelewa ni kwa nini wanafanya mambo kwa njia tofauti. Na kadiri urafiki wetu unavyokuwa wa karibu zaidi, tunaacha kukazia tofauti tulizonazo. Tunaanza kuwathamini zaidi, wanapokuwa na shangwe, tunashangilia nao, na wanapokuwa na huzuni tunahuzunika nao.

Mfikirie mwanamke anayeitwa Nazaré. Wakati fulani alikuwa akiwabagua wahamiaji. Anaeleza jambo lililomsaidia. Anasema: “Nilishirikiana nao na kufanya kazi pamoja nao. Watu hao walikuwa tofauti kabisa na mambo ambayo watu wengine walisema kuwahusu. Unapofanya urafiki na watu wa jamii tofauti, unaanza kuwapenda, kuwathamini na kuelewa kwamba kila mmoja wao ana sifa tofauti na mwenzake.”

Mambo Unayoweza Kufanya

Tafuta fursa za kuzungumza na watu kutoka nchi, kabila au lugha nyingine. Unaweza:

  • Kuwaomba wakueleze kuhusu maisha yao.

  • Kuwakaribisha kwa ajili ya chakula.

  • Kusikiliza kwa makini wanapokusimulia kuhusu maisha yao na kutambua mambo wanayoona kuwa muhimu.

Ukielewa jinsi mambo waliyopitia maishani yalivyowaathiri, huenda ukawa na mtazamo mzuri.