Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Hadithi ya Kwanza ya Uwongo: Nafsi Haifi

Hadithi ya Kwanza ya Uwongo: Nafsi Haifi

Hadithi ya Kwanza ya Uwongo: Nafsi Haifi

Ni nini chanzo cha hadithi hiyo? “Wanafalsafa wa mapema ambao walikuwa Wakristo walikubali fundisho la Wagiriki la kwamba nafsi haiwezi kufa na walifikiri kwamba nafsi inaumbwa na Mungu na kutiwa ndani ya mwili wakati wa kuzaliwa.”—The New Encyclopædia Britannica (1988), Buku la 11, ukurasa wa 25.

Biblia inasema nini? “Nafsi inayofanya zambi, itakufa.”—Ezekieli 18:4, Zaire Swahili Bible.

Kuhusu kuumbwa kwa nafsi ya kwanza ya mwanadamu, Biblia inasema hivi: “Yehova Mungu akamfanya mtu kutoka katika mavumbi ya nchi na kupuliza katika mianzi ya pua yake pumzi ya uhai, naye mtu akawa nafsi hai [Kiebrania, neʹphesh].”—Mwanzo 2:7.

Neno la Kiebrania neʹphesh, linalotafsiriwa “nafsi,” linamaanisha ‘kiumbe kinachopumua.’ Mungu alipomuumba mwanadamu wa kwanza Adamu, hakutia ndani ya mwanadamu huyo nafsi isiyoweza kufa lakini alitia ndani yake nguvu ya uhai ambayo inaendelezwa kwa kupumua. Kwa hiyo, neno “nafsi” katika Biblia linamaanisha kwa ujumla kiumbe hai. Nafsi ikitenganishwa na nguvu ya uhai ambayo ilitoka kwa Mungu, nafsi hiyo inakufa.—Mwanzo 3:19; Ezekieli 18:20.

Fundisho la kwamba nafsi haifi linatokeza maswali: Nafsi zinaenda wapi baada ya kifo? Nafsi za waovu zinapatwa na nini? Wakati watu waliodai kuwa Wakristo walipokubali hadithi ya uwongo ya kwamba nafsi haifi, hilo liliwafanya wakubali hadithi nyingine ya uwongo, yaani, fundisho la moto wa mateso.

Linganisha mistari hii ya Biblia: Mhubiri 3:19; Mathayo 10:28; Matendo 3:23

UKWELI:

Baada ya kifo mtu haendelei kuishi