Hamia kwenye habari

Mwanzilishi wa Mashahidi wa Yehova Ni Nani?

Mwanzilishi wa Mashahidi wa Yehova Ni Nani?

 Tengenezo la kisasa la Mashahidi wa Yehova lilianza mwishoni mwa karne ya 19. Wakati huo, kikundi kidogo cha wanafunzi wa Biblia walioishi karibu na Pittsburgh, Pennsylvania, Marekani, walianza kuchunguza Biblia kwa mpangilio. Walilinganisha mafundisho ya makanisa na kile ambacho Biblia inafundisha hasa. Walianza kuchapisha habari walizojifunza katika vitabu, magazeti, na jarida ambalo sasa linaitwa Mnara wa Mlinzi—Unaotangaza Ufalme wa Yehova.

 Katikati ya kikundi hicho cha wanafunzi wa Biblia wenye unyoofu kulikuwa na mwanamume aliyeitwa Charles Taze Russell. Ingawa Russell alichukua uongozi katika kazi ya kufundisha Biblia wakati huo na alikuwa ndiye mhariri wa kwanza wa gazeti Mnara wa Mlinzi, hakuwa mwanzilishi wa dini mpya. Kusudi la Russell na wenzake ambao wakati huo walikuwa wakiitwa Wanafunzi wa Biblia, lilikuwa kuendeleza mafundisho ya Yesu Kristo na kufuata mfano wa kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza. Kwa kuwa Yesu ndiye Mwanzilishi wa Ukristo, tunamwona yeye kuwa mwanzilishi wa tengenezo letu.—Wakolosai 1:18-20.