Hamia kwenye habari

Makusanyiko ya Pekee ya Mashahidi wa Yehova Yalifanywa Katika Nchi Saba

Makusanyiko ya Pekee ya Mashahidi wa Yehova Yalifanywa Katika Nchi Saba

Hivi karibuni Mashahidi wa Yehova walifanya makusanyiko ya pekee katika nchi za Brazili, Kosta Rika, Hong Kong, Ireland, Israel, New Zealand, na Sweden. Kusanyiko la kwanza, lilifanywa nchini Sweden mnamo Julai 2012, makusanyiko matatu ya mwisho yalifanywa nchini Kosta Rika na New Zealand mnamo Januari 2013.

Kama ilivyo na makusanyiko mengine ya siku tatu ambayo yamewahi kupangwa, makusanyiko haya yalikazia sana hotuba za Biblia, maonyesho, na drama.

Kwa ajili ya makusanyiko haya ya pekee, wajumbe walikaribishwa ili wahudhurie nje ya nchi wanakotoka. Kabla na baada ya makusanyiko hayo, wahudhuriaji walikuwa na nafasi ya kuwa na matembezi yaliyopangwa mapema na nchi iliyowakaribisha.

Mwanamume mmoja aliyehudhuria kusanyiko lililofanyika huko Brazili alisema hivi: “Nilisisimka sana kushuhudia upendo wa kipekee na ukarimu ambao akina ndugu walionyeshana. Ni kana kwamba nilipata familia ya kweli.”

Mwanamume mwingine aliyehudhuria kusanyiko la pekee katika nchi ya Hong Kong, alisema hivi: “Nilivutiwa sana kuona nyuso zenye shangwe na tabasamu nyingi wakati wajumbe wanaozungumza lugha ya Mandarin walipokumbatia kifuani mwao Biblia mpya iliyotolewa.”

Kila mwaka, Mashahidi wa Yehova wanafanya Makusanyiko kotekote ulimwenguni, na mamilioni wanahudhuria

Makusanyiko yanatoa nafasi kwa wale waliohudhuria kujionea upendo, shangwe, na amani miongoni mwa akina ndugu. Jambo hilo linaonekana wazi katika makusanyiko ya pekee na ya kimataifa. Katika makusanyiko hayo, wajumbe wanazungumza kwa furaha na kula pamoja, wanabadilishana zawadi kidogo na anwani, kupiga picha, na kukumbatiana kwa uchangamfu mwingi wakati wa mapumziko.

Katika makusanyiko yetu, kila mtu hata wale ambao si Mashahidi wa Yehova, wanaalikwa kuhudhuria.