Ona video zinazopatikana

Biblia Inasema Nini juu ya Mutu Kujichanja Alama Kwenye Mwili?

Biblia Inasema Nini juu ya Mutu Kujichanja Alama Kwenye Mwili?

Jibu la Biblia

 Biblia inazungumuzia kujichanja alama kwenye mwili mara moja tu, katika andiko ya Mambo ya Walawi 19:28, yenye inasema hivi: “Hamupaswe kujitia alama za machanjo.” Kwa kuwatolea Waisraeli amri hii, Mungu alipenda wakuwe tofauti na watu wa mataifa jirani wenye walichora kwenye miili yao majina ao alama za miungu yao. (Kumbukumbu la Torati 14:2) Hata kama Wakristo hawako chini ya Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli, wanaweza kufikiria kwa uzito kanuni yenye kutegemeza ile sheria.

Mukristo anaweza kujichanja ao kuchorwa alama kwenye mwili?

 Maandiko ya Biblia yenye kuwa hapa chini inaweza kukusaidia kuamua:

  •   “Wanamuke wajipambe . . . kwa kiasi.” (1 Timoteo 2:9) Hii kanuni inaweza kusaidia wanamuke na wanaume. Tunapaswa kuhangaikia maoni ya wengine na kuepuka kujionyesha.

  •   Watu fulani wanajichanja alama kwenye mwili ili kujitambulisha ao kuonyesha kama wako huru, na wengine wanajichanja alama kwenye mwili ili kuonyesha kama wako huru kutendea mwili wao namna wanataka. Lakini, Biblia inashauri Wakristo hivi: “Mutoe miili yenu ikuwe zabihu yenye uzima, takatifu, na yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mutakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri.” (Waroma 12:1) Tumia ‘nguvu zako za kufikiri’ na ujiulize sababu gani unataka kujichanja alama kwenye mwili. Ni kwa sababu unataka kufuata mutindo fulani? Ao unataka kuonyesha kama uko katika kikundi fulani? Kumbuka kama unaweza kubadilisha mawazo yako, lakini hauwezi kuondoa chanjo kwenye mwili wako. Kuchunguza sababu zenye zinakuchochea kunaweza kukusaidia uchukue uamuzi muzuri.—Mezali 4:7.

  •   “Mipango ya wenye bidii hakika inaleta mafanikio, Lakini wale wote wenye kutenda haraka-haraka hakika watakuwa maskini.” (Mezali 21:5) Mara mingi watu wanaamua haraka-haraka kujichanja alama kwenye mwili; lakini wanasahau kama kufanya vile kunaweza kuwa na matokeo ya mubaya juu ya uhusiano wao na wengine, na juu ya kazi yao. Tena, kwa kawaida kujichanja alama kwenye mwili kunaomba feza mingi, na kunaumiza sana. Habari mbalimbali na biashara yenye kuendelea sana juu ya kuondoa alama za kujichanja kwenye mwili, inaonyesha kama watu mingi wenye wamejichanja alama kwenye mwili wanafikia kusikitika.