Ona video zinazopatikana

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kasirani?

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kasirani?

Jibu ya Biblia

 Biblia inafundisha kama kasirani yenye haizuiwe inaweza kuwa na matokeo ya mubaya juu ya mutu mwenye kuwa nayo na juu ya wale wenye kumuzunguka. (Mezali 29:22) Hata kama wakati fulani mutu anaweza kuwa na sababu ya kukasirika, Biblia inasema kama wale wenye wanaendelea kuwa na “milipuko ya kasirani” hawatapata wokovu. (Wagalatia 5:19-​21) Biblia iko na kanuni zenye zinaweza kusaidia mutu kupiganisha kasirani.

 Kila wakati njo inakuwaka mubaya kukasirika?

 Hapana. Mu hali fulani, mutu anaweza kuwa na sababu ya kukasirika. Kwa mufano, Nehemia mwanaume mukamilifu ‘alikasirika sana’ wakati alisikia kilio ya waabudu wenzake wenye walikuwa wanatendewa mubaya.​—Nehemia 5:6.

 Wakati fulani, Mungu alikasirika. Kwa mufano, wakati watu wake wa zamani waliacha kumuabudu tu yeye na kuanza kutumikia miungu ya uongo “kasirani ya Yehova ikawaka juu” yao. (Waamuzi 2:13, 14) Hata vile, Yehova Mungu hakasirikake ovyoovyo. Sikuzote anakuwaka na sababu ya kukasirika na anajuaka namna ya kuzuia kasirani yake.​—Kutoka 34:6; Isaya 48:9.

 Ni wakati gani njo mubaya kukasirika?

 Ni mubaya kukasirika wakati mutu anashindwa kuzuia kasirani yake ao wakati mutu anakasirika bila sababu yoyote. Mara mingi kasirani ya vile inafikiaka wanadamu wenye hawakamilike. Kwa mufano:

  •   Kaini ‘alikasirika sana’ wakati Mungu hakukubali toleo yake. Kaini aliacha kasirani yake imufanye afikie kuua ndugu yake.​—Mwanzo 4:3-8.

  •   Nabii Yona ‘alikasirika sana’ wakati Mungu alisikilia huruma watu wa Ninawi. Mungu alimurekebisha Yona kwa kumuambia kama hakukuwa na “sababu ya kukasirika vile” na kama alipaswa kusikilia huruma wale watenda-zambi wenye walitubu.​—Yona 3:10–​4:1, 4, 11. *

 Hii mifano inaonyesha kama kwa wanadamu wenye hawakamilike, ‘kasirani haitokeze haki ya Mungu.’​—Yakobo 1:20.

 Namna gani unaweza kupiganisha kasirani?

  •   Utambue hatari ya kushindwa kuzuia kasirani. Watu fulani wanaweza kuwaza kama mutu mwenye anaonyesha kasirani yake maana yake iko na nguvu. Kusema kweli, mutu mwenye hawezi kuzuia kasirani yake iko na uzaifu mukubwa sana. Biblia inasema hivi: “Kama muji wenye umebomolewa, wenye hauna ukuta ni vile pia mutu mwenye hawezi kuzuia kasirani yake.” (Mezali 25:28; 29:11) Kwa upande mwingine, kama tunajikaza kuzuia kasirani yetu, tunaonyesha kabisa kama tuko na nguvu na utambuzi. (Mezali 14:29) Biblia inasema hivi: “Mutu mwenye hakasirike haraka ni muzuri zaidi kuliko mwanaume mwenye nguvu.”​—Mezali 16:32.

  •   Upiganishe kasirani yako mbele ikuchochee kufanya jambo fulani yenye utahuzunikia kisha. Zaburi 37:8 inasema hivi: “Acha hasira na uache kasirani kali; usikasirike na kuanza kutenda uovu.” Usisahau kama wakati unakasirika, uko na uamuzi, ni kusema, wa kuacha kukasirika mbele ya “kutenda uovu.” Sawa vile Waefeso 4:26 inasema, “mukuwe na kasirani, lakini musitende zambi.”

  •   Kama inawezekana, ondoka wakati kasirani inaanza kupanda. Biblia inasema hivi: “Kuanzisha vita ni kama kufungua mulango mukubwa wa mafuriko; mbele ugomvi uanze, ondoka.” (Mezali 17:14) Hata kama ni jambo ya hekima kufanya amani na wengine haraka, inaweza kuwa muzuri kwanza weye na ule mutu mwingine mutulie mbele ya kuzungumuzia ile jambo.

  •    Ukuwe na habari zote. Mezali 19:11 inasema hivi: “Ufahamu wa mutu hakika unatuliza kasirani yake.” Tutaonyesha kama tuko na hekima, kama tuko na habari zote mbele ya kuamua jambo fulani. Wakati tunasikiliza kwa uangalifu pande zote mbili, itatusaidia tusikasirike bila sababu.​—Yakobo 1:19.

  •    Usali ili kupata amani ya akili. Sala inaweza kukusaidia kupata “amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote.” (Wafilipi 4:7) Sala ni njia moya kati ya njia zenye zinaweza kutusaidia kupata roho takatifu ya Mungu yenye inaweza kufanya tukuwe na sifa sawa vile, amani, uvumilivu, na kujizuia.​—Luka 11:13; Wagalatia 5:22, 23.

  •   Uchague kwa uangalifu marafiki wako. Tunakuwaka na muelekeo wa kuwa sawa vile marafiki wetu. (Mezali 13:20; 1 Wakorinto 15:33) Njo maana, Biblia inatuambia hivi: “Usishirikiane na mutu mwenye kukasirika-kasirika wala kujiunga na mutu mwenye muelekeo wa kukasirika sana.” Juu ya nini? “Ili usijifunze hata kidogo njia zake na kujitia katika mutego.”​—Mezali 22:24, 25.

^ Inaonekana Yona alikubali kurekebishwa na aliacha kukasirika, juu Mungu alimutumia ili kuandika kitabu ya Biblia yenye kuwa na jina ya Yona.