Ona video zinazopatikana

Juu ya Nini Hakuna Amani mu Dunia?

Juu ya Nini Hakuna Amani mu Dunia?

Jibu ya Biblia

 Wanadamu wamefanya yao yote juu ya kuleta amani, lakini wapi! Na kusema kweli, hawataweza kuleta amani juu ya sababu zenye kufuata:

  •   “Mwanadamu mwenye kutembea hana hata uwezo wa kuongoza hatua yake.” (Yeremia 10:23) Wanadamu hawakuumbwa na uwezo ao haki ya kujiongoza wao wenyewe, kwa hiyo hawana uwezo wa kuleta amani ya milele.

  •   “Musitumainie wakubwa wala mwana wa binadamu, mwenye hawezi kuleta wokovu. Roho yake inatoka, anarudia kwenye udongo; siku ileile mawazo yake yanapotea.” (Zaburi 146:3, 4) Viongozi wa serikali, hata wale wenye kuwa na nia ya muzuri, hawana uwezo wa kutosha mambo yenye kuleta vita.

  •   “Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia. Kwa maana watu watakuwa . . . wakali, wenye hawapendi wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi.” (2 Timoteo 3:1–4) Tuko naishi mu “siku za mwisho” za hii dunia, mu wakati yenye tabia za watu zinafanya ikuwe nguvu kupata amani.

  •   “Ole wa dunia na wa bahari, kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na kasirani kali, akijua kwamba iko na kipindi kifupi cha wakati.” (Ufunuo 12:12) Ibilisi, adui ya Mungu, alishatupwa mu ujirani wa dunia na anachochea watu wakuwe na roho ya mubaya sana sawa yeye. Kama yeye angali tu “mutawala wa ulimwengu huu,” hatuwezi kuishi kwa amani.​—Yohana 12:31.

  •   “[Ufame wa Mungu] utaponda na kumaliza falme hizi zote, na ufalme huo peke yake utasimama milele.” (Danieli 2:44) Ufalme wa Mungu njo utatimiza tamaa yetu ya kuwa na dunia yenye amani milele, hapana serikali za wanadamu.​—Zaburi 145:16.