Ona video zinazopatikana

Kuvuta Tumbako Ni Zambi?

Kuvuta Tumbako Ni Zambi?

Jibu ya Biblia

 Biblia haizungumuzie kuvuta tumbako * ao njia zingine za kutumia tumbako. Lakini iko na kanuni zenye kuonyesha kama Mungu anachukia mazoea machafu yenye kuharibisha afya, njo maana kwake, kuvuta tumbako ni zambi.

  •   Kuheshimia uzima. “Mungu . . . anapatia watu wote uzima na pumuzi na vitu vyote.” (Matendo 17:24, 25) Kwa kuwa uzima ni zawadi kutoka kwa Mungu, hatupaswe kufanya jambo yoyote yenye inaweza kufupisha maisha yetu, kama vile kuvuta tumbako. Kuvuta tumbako iko kati ya mambo ya nguvu yenye inatokeza vifo vyenye vingeweza kuzuiliwa mu dunia.

  •   Kupenda jirani. “Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.” (Matayo 22:39) Kuvuta tumbako pembeni ya watu wengine, kunaonyesha kama hauwapendi. Watu wenye kwa ukawaida wanapumua moshi kutoka kwa mutu mwenye kuvuta tumbako, wako mu hatari sana ya kupata ileile ugonjwa yenye mara mingi inapataka wavuta-tumbako.

  •   Ulazima wa kuwa mutakatifu. “Mutoe miili yenu ikuwe zabihu yenye uzima, takatifu, na yenye kukubalika kwa Mungu.” (Waroma 12:1) “Tujisafishe kila uchafu wa mwili na roho, tukikamilisha utakatifu katika kumuogopa Mungu.” (2 Wakorinto 7:1) Kuvuta tumbako haiko jambo ya asili na haipatane na kuwa mutakatifu, ni kusema, kitu safi na yenye kutakata. Juu watu wenye kutumia tumbako wanaingiza kwa makusudi mu mwili yao sumu yenye inaweza kuharibu mwili yao.

Biblia inasema jambo fulani juu ya kutumia bangi ao dawa zingine za kulewesha?

 Biblia haizungumuzie bangi ao dawa zingine za kulewesha. Lakini iko na kanuni zenye kuonyesha kama haifae kutumia vitu kama vile vyenye vinafanya mutu akuwe mutumwa. Zaidi ya zile kanuni zenye tulizungumuzia, hizi ni kanuni zingine zenye zinatumika mu hii hali:

  •   Ulazima wa kulinda uwezo wetu wa kufikiri. “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako . . . kwa akili yako yote.” (Matayo 22:37, 38) “Mulinde akili zenu kwa ukamili.” (1 Petro 1:13) Mutu hawezi kulinda muzuri akili yake wakati iko anatumia dawa kwa njia ya mubaya. Watu wengi hata wanakuwa watumwa wa zile dawa. Akili yao inakuwa tu inawaza namna ya kupata na kutumia dawa za kulewesha kuliko kukaza akili juu ya mawazo yenye kujenga.​—Wafilipi 4:8.

  •   Kutii sheria za serikali. “[Watii] serikali na mamlaka.” (Tito 3:1) Mu mainchi ya mingi, sheria zinakataza kabisa kutumia dawa fulani. Kama tunataka kumupendeza Mungu, tunapaswa kutii sheria za serikali.​—Waroma 13:1.

^ Hapa, kuvuta maana yake kukokota kwa makusudi moshi ya tumbako ao ya paipo. Lakini kanuni zenye tutazungumuzia zinahusu pia kutafuna majani ya tumbako ao kutumia kwa njia ya kielektroniki tumbako yenye kuwa na nicotine na vitu vingine sawa ile.