Ona video zinazopatikana

Je, Mukristo Anaweza Kukubali Matunzo ya Kiganga?

Je, Mukristo Anaweza Kukubali Matunzo ya Kiganga?

Jibu la Biblia

 Ndiyo. Yesu alionyesha kwamba wafuasi wake wanaweza kutafuta matunzo ya kiganga aliposema kwamba ‘watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomuhitaji ni wale walio wagonjwa.’ (Mathayo 9:12, BIBLIA HABARI NJEMA) Biblia si kitabu cha kiganga, lakini inatoa kanuni zinazoweza kuwasaidia wale wanaotaka kumupendeza Mungu.

Maulizo unayopaswa kufikiria

 1. Je, ninaelewa matunzo ambayo ninashauriwa kupata? Biblia inatushauri tutafute muongozo muzuri kuliko ‘kuamini kila neno.’—Methali 14:15.

 2. Je, nitafute mashauri kwa waganga wengine? Ndiyo, kuwauliza “washauri wengi” kunaweza kukusaidia, zaidi sana ikiwa umegonjwa sana.—Methali 15:22.

 3. Je, aina hii ya matunzo inapingana na sheria ya Mungu inayowaomba Wakristo “wajiepushe . . . na damu”?—Matendo 15:20.

 4. Je, aina hii ya matunzo ina uhusiano na mambo ya uchawi? Biblia inakataza “mazoea ya kuwasiliana na pepo.” (Wagalatia 5:19-21) Ili kujua ikiwa inahusiana na uchawi, jiulize maulizo haya:

  •   Je, muganga huyu wa kienyeji anazungumuza na mashetani?

  •   Je, aina hii ya matunzo inategemea maoni ya kwamba magonjwa yanatokea kwa sababu miungu imekasirika ao kwa sababu ya maadui wanaotumia uchawi?

  •   Je, zabihu, nyimbo za uchawi, ao desturi zingine za kupashana habari na mashetani zinatumiwa wakati wa kutengeneza dawa hiyo?

 5. Je, nimeanza kuhangaikia afya yangu kupita kiasi? Biblia inashauri hivi: “Usawaziko wenu na ujulikane kwa watu wote.” (Wafilipi 4:5) Kuwa mwenye usawaziko kutakusaidia ukazie uangalifu “mambo yaliyo ya maana zaidi,” kama vile mambo ya kiroho.—Wafilipi 1:10; Mathayo 5:3.