Ona video zinazopatikana

Mungu Anakuwaka?

Mungu Anakuwaka?

Jibu ya Biblia

 Ndiyo, mu Biblia muko ushuhuda wenye kuonyesha kabisa kama Mungu anakuwaka. Biblia inatutia moyo tumuamini Mungu. Ile haimaanishe kama tunapaswa tu kuitika-itika mambo yenye makanisa inafundisha. Lakini tunapaswa kutumia ‘nguvu zetu za kufikiri’ na “uwezo [wetu] wa kufikiri.” (Waroma 12:1; 1 Yohana 5:20, maelezo ya chini) Ona ushuhuda fulani wenye Biblia inatoa:

  •   Ulimwengu wenye kupangwa muzuri na pia vitu vyenye kuwa ndani vinaonyesha kama kuko Muumbaji. Biblia inasema hivi: “Kwa kweli, kila nyumba inajengwa na mutu fulani, lakini ule mwenye alijenga vitu vyote ni Mungu.” (Waebrania 3:4) Hata kama mawazo ya ile andiko ni ya mwepesi, watu wengi wenye elimu wanaona kama ni mawazo yenye mutu hawezi kupinga. *

  •   Siye wanadamu tunazaliwa na tamaa ya kutafuta kujua juu ya nini tuko ku dunia. Tunaendelea kuwa na ile tamaa hata kisha kutimiza mahitaji yetu ya kimwili. Biblia inaita ile tamaa kuwa ‘uhitaji wa kiroho.’ Ule uhitaji unatia ndani pia tamaa ya kumujua Mungu na kumuabudu. (Matayo 5:3; Ufunuo 4:11) Vile tuko na ile tamaa, ile inaonyesha kama Mungu iko na kama ni Muumbaji mwenye upendo na anapenda tutimize ile tamaa.​—Matayo 4:4.

  •   Mu Biblia muko maunabii yenye iliandikwa zamani sana na ilifikia kutimia kabisa sawa vile tu Biblia ilikuwaka ilishasema. Juu ile maunabii ilitimia kabisa, ile inaonyesha kama mwenye aliisemaka iko na uwezo sana kupita wanadamu.​—2 Petro 1:21.

  •   Waandikaji wa Biblia walijua mambo ya sayansi yenye watu wenye walikuwa wanaishi ile wakati hawakukuwa wanajua. Kwa mufano, zamani watu wengi waliamini kama dunia inaikala juu ya munyama fulani, sawa vile tembo, nguruwe ya pori, ao ngombe dume. Lakini, Biblia inasema kama Mungu “ananinginiza dunia mahali kwenye hakuna kitu.” (Yobu 26:7) Vilevile, Biblia inafasiria muzuri umbo ya dunia. Inasema kama dunia iko “muviringo.” (Isaya 40:22) Watu wengi wanaona kama inapaswa tu kuwa Mungu njo alisaidia waandikaji wa Biblia waelewe zile habari.

  •   Biblia inajibia maulizo mingi ya nguvu sana, yenye kama haijibiwe muzuri inaweza kufanya mutu asiamini kama Mungu anakuwaka. Kwa mufano: Kama Mungu iko na upendo na iko na nguvu sana, juu ya nini anaacha mateso na mambo ya mubaya iendelee mu dunia? Juu ya nini mara mingi makanisa inachocheaka watu wafanye mambo ya mubaya, kuliko kuwachochea wafanye mambo ya muzuri?​—Tito 1:16.

^ Kwa mufano, Allan Sandage, mwenye alikuwaka anajifunza mambo ya astronomia, alisemaka hivi kuhusu ulimwengu: “Siamini kabisa kama ulimwengu wenye kupangwa muzuri sana ulijitokeza wenyewe. Kunapaswa kuwa mutu mwenye aliupanga vile. Miye sijue kama Mungu anakuwaka. Lakini vitu vyenye kuwa mu ulimwengu vinaonyesha kama kunapaswa kuwa muumbaji.”