Ona video zinazopatikana

Mutu Anakuwa Katika Hali Gani Anapokufa?

Mutu Anakuwa Katika Hali Gani Anapokufa?

Jibu la Biblia

 Biblia inasema hivi: “Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe.” (Mhubiri 9:5; Zaburi 146:4) Kwa hiyo, tunapokufa hatuendelee kuishi. Wafu hawawezi kuwaza, kutenda ao kufanya jambo lolote.

“Utarudi mavumbini”

 Alipozungumuza na mwanaume wa kwanza, Adamu, Mungu alionyesha hali ya mutu ambaye amekufa. Adamu hakumutii Mungu, kwa hiyo Mungu alimuambia hivi: “Wewe ni mavumbi nawe utarudi mavumbini.” (Mwanzo 3:19) Mbele Mungu amuumbe Adamu ‘kutoka katika mavumbi ya inchi,’ Adamu hakuwa anaishi. (Mwanzo 2:7) Vivyo hivyo, Adamu alipokufa, alirudi katika mavumbi na maisha yake yaliishia hapo.

 Hiyo ndio hali ya wale wanaokufa leo. Kuhusu watu na wanyama, Biblia inasema hivi: “Wote wametoka katika mavumbi, nao wote wanarudi mavumbini.”​—Mhubiri 3:19, 20.

Kifo si mwisho wa mambo yote

 Biblia inalinganisha kifo na usingizi. (Zaburi 13:3; Yohana 11:11-14; Matendo 7:60) Mutu anayelala usingizi muzito hawezi kujua jambo lolote linalofanywa pembeni yake. Vivyo hivyo, wafu hawajue jambo lolote. Lakini, Biblia inafundisha kwamba Mungu anaweza kuwaamusha wale waliokufa kama kumuamusha mutu katika usingizi na kuwarudishia uzima. (Ayubu 14:13-15) Kwa wale ambao Mungu atafufua, kifo si mwisho wa mambo yote.