Ona video zinazopatikana

Sayansi Inapatana na Biblia?

Sayansi Inapatana na Biblia?

Jibu la Biblia

 Ni ndiyo. Hata ikiwa Biblia haiko kitabu cha sayansi inasema kweli inapozungumuzia mambo ya sayansi. Fikiria mifano fulani inayoonyesha kwamba sayansi na Biblia vinapatana na kwamba Biblia ina mawazo fulani ya kweli yanayopatana na sayansi ambayo yanatofautiana kabisa na mawazo ya watu wengi ambao waliishi wakati iliandikwa.

  •   Ulimwengu ulikuwa na mwanzo. (Mwanzo 1:1) Hata hivyo, hadisi za uongo za zamani zilionyesha kwamba ulimwengu haukuumbwa, lakini ulijitokeza wenyewe kutokana na muchafuko mukubwa uliokuwa wakati huo. Wababiloni waliamini kwamba miungu iliyozaa ulimwengu ilitoka katika bahari mbili. Hadisi zingine za uongo zilionyesha kwamba ulimwengu ulitoka katika yai moja kubwa.

  •   Ulimwengu unaongozwa na sheria za asili zilizowekwa na mutu mwenye akili, haiongozwe na mawazo ya miungu. (Ayubu 38:33; Yeremia 33:25) Hadisi za uongo katika dunia yote zinaonyesha kwamba wanadamu hawawezi kuepuka matendo yasiyotazamiwa na yasiyo na huruma ya miungu.

  •   Dunia imetundikwa katika anga. (Ayubu 26:7) Zamani, watu wengi waliamini kwamba dunia ilikuwa diske iliyoshikiliwa na kiumbe fulani kikubwa sana ao munyama mukubwa kama vile, tembo ao kasa wa bahari.

  •   Maji ya mito na chemichemi yanatokana na maji ya bahari ambayo yamegeuka kuwa muvuke ao inatokana na vyanzo vingine, na kisha yananyesha kama mvua, teluji ao mvua wa majiwe. (Ayubu 36:27, 28; Muhubiri 1:7; Isaya 55:10; Amosi 9:6) Wagiriki wa zamani walifikiri kwamba maji ya mito yanatoka katika bahari iliyo chini ya udongo, na wazo hili liliendelea mupaka miaka ya 1701-1800.

  •   Milima inainuka na kuzama, na milima ya leo ilikuwa siku moja inafunikwa na bahari. (Zaburi 104:​6, 8) Lakini, hadisi nyingi za uongo zinasema kwamba milima iliumbwa na miungu katika hali yake ya leo.

  •   Usafi unasaidia kuwa na afya nzuri. Sheria ambayo Waisraeli walipewa ilizungumuzia mambo kama vile kufua nguo kisha kugusa maiti, kutenga wale walio na magonjwa ya kuambukiza, na kufunika vizuri mavi ya mutu. (Walawi 11:28; 13:1-5; Kumbukumbu la Torati 23:13) Lakini, sheria hizo zilipotolewa kulikuwa njia moja ya matunzo katika Misri iliyowaomba watu watunze vidonda kwa kutumia dawa fulani iliyochanganywa na mavi ya mutu.

Biblia Inafundisha Mambo Fulani Ambayo Hayapatane na Sayansi?

 Uchunguzi muzuri wa Biblia unaonyesha kwamba jibu ni hapana. Ona mawazo fulani ya uongo ambayo yameenea juu ya Biblia:

 Uongo: Biblia inasema kwamba ulimwengu uliumbwa kwa siku sita, kila siku ilikuwa na saa 24.

 Ukweli: Biblia inaonyesha kwamba Mungu aliumba ulimwengu zamani, lakini haijulikane ilikuwa wakati gani. (Mwanzo 1:1) Pia, siku za uumbaji zinazozungumuziwa katika sura ya 1 ya Mwanzo zilikuwa vipindi vya wakati, urefu wa vipindi hivyo haujulikane. Vilevile, muda wote ambao uumbaji wa dunia na mbingu ulichukua unaitwa pia “siku” moja.​—Mwanzo 2:4.

 Uongo: Biblia inasema kwamba mimea iliumbwa mbele ya jua kuumbwa ili ifanye kazi na mufumo unaoitwa usanidimwanga (photosynthèse).​—Mwanzo 1:​11, 16.

 Ukweli: Biblia inaonyesha kwamba jua, ambayo ni moja ya nyota zilizo katika “mbingu,” iliumbwa mbele ya mimea. (Mwanzo 1:1) Katika “siku” (ao kipindi) ya kwanza ya uumbaji, mwangaza wenye kufifia wa jua ulifika kwenye dunia. Kama vile angahewa ilivyoendelea kuwa wazi mwishoni mwa “siku” ya tatu ya uumbaji, mwangaza wa jua ulikuwa nguvu ili kuendesha mufumo wa usanidimwanga. (Mwanzo 1:​3-5, 12, 13) Ni muda fulani baadaye tu ndipo mutu aliye kwenye dunia angeweza kuona jua waziwazi.​—Mwanzo 1:​16.

 Uongo: Biblia inasema kwamba jua inazunguka juu ya dunia.

 Ukweli: Muhubiri 1:5 inasema hivi: “Jua limechomoza, na kushuka, nalo linajitahidi kwa nguvu kwenda mahali pake ambapo litachomoza tena.” Lakini, maneno hayo yanazungumuzia tu mwendo wa jua namna unavyoonwa na mutu aliye kwenye dunia. Hata leo, mutu anaweza kusema “jua linaamuka” na “jua linalala,” lakini anajua kwamba dunia ndiyo inazunguka juu ya jua.

 Uongo: Biblia inasema kwamba dunia ni tambarare.

 Ukweli: Biblia inatumia maneno kama vile “mwisho wa dunia” ili kumaanisha “sehemu ya mbali zaidi ya dunia”; maneno hayo hayaonyeshe kwamba dunia ni tambarare. (Matendo 1:8) Vile vile, maneno “miisho minne ya dunia” ni usemi wa mufano unaohusu eneo lote la dunia; leo mutu anaweza kutumia kwa njia ya mufano maneno kama vile Mashariki, Mangaribi, Kaskazini, na Kusini.​—Isaya 11:12; Luka 13:29.

 Uongo: Biblia inasema kwamba duara la miviringo ni mara tatu kipenyo ao diametre yake, lakini kwa kweli ni pi (π), ao karibu 3.1416.

 Ukweli: Vipimo vya “Bahari ya kuyeyushwa” vilivyo kwenye 1 Wafalme 7:23 na 2 Mambo ya Nyakati 4:2 vinaonyesha kwamba bahari hiyo ilikuwa na kipenyo cha mikono 10 na “kamba ya urefu wa mikono 30 ingeweza kuizunguka pande zote.” Inawezekana vipimo hivyo vilikuwa tu nambari kamili zenye kukaribiana. Pia, inawezekana duara na kipenyo zilionyesha vipimo vya ndani na vya inje vya bahari hiyo.