Ona video zinazopatikana

Shetani Anaishi Wapi?

Shetani Anaishi Wapi?

Jibu la Biblia

 Kwa kuwa yeye ni kiumbe wa kiroho, Shetani anaishi katika ulimwengu usioonekana. Lakini, huo si ulimwengu wa moto wa mateso ambako anawatesa watu wabaya, kama unavyoweza kuona kwenye picha inayopatikana katika habari hii.

“Vita mbinguni”

 Wakati fulani, Shetani Ibilisi alikuwa na uhuru wa kuzunguka mbinguni, na kwenda hata mbele za Yehova pamoja na malaika waaminifu. (Ayubu 1:6) Lakini Biblia ilitabiri kwamba kungetokea “vita mbinguni” na Shetani angefukuzwa mbinguni na ‘kutupwa duniani.’ (Ufunuo 12:7-9, Verbum Bible) Historia ya Biblia na mambo yaliyotokea katika ulimwengu yanahakikisha kwamba vita hiyo imekwisha kutokea mbinguni. Sasa amezuiwa kwenye ujirani wa dunia.

 Je, hilo linamaanisha kwamba Shetani anaishi mahali fulani katika dunia yetu? Fikiria mufano huu: Biblia inasema kwamba muji wa zamani wa Pergamamu ulikuwa “mahali kilipo kiti cha ufalme cha Shetani” na “mahali anapokaa Shetani.” (Ufunuo. 2:13) Kwa kweli, maneno hayo yalimaanisha mahali ambapo watu waliabudu sana Shetani katika muji huo. Biblia inasema kwamba Shetani anaitawala “falme zote za dunia inayokaliwa,” kwa hiyo haishi mahali fulani duniani lakini anapatikana tu katika ujirani wa dunia.​—Luka 4:​5, 6.