Ona video zinazopatikana

VIJANA WANAULIZA

Namna Gani Naweza Kuchagua Mufano Muzuri wa Kuiga?

Namna Gani Naweza Kuchagua Mufano Muzuri wa Kuiga?

 “Wakati nilipata magumu kwenye masomo, kufikiria mutu fulani mwenye nilifurahia na mwenye alipatwa na hali kama yangu, kulinisaidia. Kisha, nilijikaza kufuata mufano wake. Kuwa na mufano muzuri wa kuiga kulinisaidia ikuwe mwepesi zaidi kupiganisha hali ngumu.”​—Haley.

 Kuwa na mufano wa kuiga kunaweza kukusaidia kuepuka matatizo na kutimiza miradi yako. Siri ni kuchagua mufano muzuri wa kuiga.

 Sababu gani uchague kwa uangalifu?

  •   Mifano ya kuiga yenye unachagua itakuwa na matokeo juu ya namna yako ya kutenda.

     Biblia inawatia moyo Wakristo kuwafikiria wale wenye kuwa mifano mizuri kwa kusema: ‘Munapotafakari jinsi mwisho wa mwenendo wao unavyokuwa, igeni imani yao.’​—Waebrania 13:7.

     Shauri: Kwa kuwa uchaguzi wako wa mifano ya kuiga utakuwa na matokeo juu yako ikuwe ni katika matendo mazuri ao mabaya, chagua watu wenye kuwa na sifa za muzuri, hapana tu watu wenye kujulikana ao wenye kuwa karibu na miaka yako.

     “Nilijifunza mambo mengi kupitia Mukristo mwenzangu mwenye kuitwa Adam, kupitia mutazamo na tabia zake kwa ujumla. Inapendeza kwamba ningali nakumbuka mambo fulani ya pekee yenye alisema na kufanya. Hajue uvutano wenye alikuwa nao juu yangu.”​—Colin.

  •   Mifano ya kuiga yenye unachagua itakuwa na matokeo juu ya mawazo na hisia zako.

     Biblia inasema hivi: ‘Musipotoshwe. Mashirika mabaya huharibu tabia nzuri.’​—1 Wakorintho 15:33.

     Shauri: Chagua mutu mwenye kuwa na sifa za muzuri, usiangalie tu sura. Tofauti na hilo, unaweza kufikia kuvunjika moyo.

     “Wakati unajilinganisha na watu wenye kuwa na sura yenye kuvutia, hilo linakufanya ujione bure kabisa na mwenye kuwa na sura ya mubaya. Linaweza kukufanya uhangaikie zaidi sura yako.”​—Tamara.

     Jambo la kufikiria: Kuchagua watu wenye kujulikana sana na wachezaji kama mifano ya kuiga kunaweza kuleta mitego gani?

  •   Mifano ya kuiga yenye unachagua inaweza kuwa na matokeo juu ya uwezekano wa kufikia miradi yako ao hapana.

     Biblia inasema hivi: “Anayetembea na watu wenye hekima atakuwa na hekima.”​—Methali 13:20.

     Shauri: Chagua mifano ya kuiga yenye kuonyesha sifa zenye unapenda kuonyesha. Kadiri unachunguza mifano hiyo, unaweza kujifunza hatua za maana zenye unaweza kukamata ili kutimiza muradi wako.

     “Kuliko kujiwekea muradi wenye hauko kamili kama vile ‘Napenda kuwa mutu mwenye kukamata mambo kwa uzito,’ unaweza kusema hivi, ‘Napenda kuwa mutu mwenye kukamata mambo kwa uzito kama vile Jane. Kila mara anaheshimia wakati na anakamata migawo yake kwa uzito.’”​—Miriam.

     Kwa kifupi: Wakati unachagua mufano muzuri wa kuiga, unalinda katika akili aina ya mutu mwenye unataka kuwa.

Kufuata mufano muzuri wa kuiga kunaweza kufanya ikuwe mwepesi kutimiza miradi yako!

 Namna ya kuchagua

 Unaweza kuchagua mufano wa kuiga katika moja ya njia zenye kuwa hapa:

  1.   Unaweza kuchagua sifa yenye unapenda kutumikia na kisha unaweza kutafuta mutu mwenye unafurahia mwenye kuwa na sifa hiyo.

  2.   Unaweza kuchagua mutu mwenye unafurahia na kisha unaweza kuchagua sifa yenye mutu huyo iko nayo ambayo unapenda kukomalisha.

Utendaji wenye kupatana na habari hii unaweza kukusaidia kufanya vile.

 Mifano yako ya kuiga inaweza kuwa:

  •  Vijana wenzako. “Rafiki wangu wa sana ni mutu mwenye napenda kuiga. Hajisikie kuwa na mambo mengi ya kufanya na kukosa hata wakati wa kusimama ili kuhangaikia mutu mwengine. Ni mutoto kidogo kuliko mimi, lakini iko na sifa yenye mimi nakosa, na hilo linanifanya nifurahie kuiga mufano wake.”​—Miriam.

  •  Watu wazima. Wanaweza kuwa wazazi wako ao watu wenye kuwa na imani kama yako. “Bila shaka, wazazi wangu ni mifano ya kuiga. Wako na sifa za muzuri sana. Najua makosa yao, lakini hata kama wako na makosa, wangali waaminifu. Natumainia kwamba wakati nitakuwa na miaka yao, nitakuwa kama wao.”​—Annette.

  •  Watu wenye kuzungumuziwa katika Biblia. “Nimechagua mifano fulani ya kuiga katika Biblia​—Timoteo, Rutu, Ayubu, Petro, mutoto mudogo mwanamuke Mwisraeli​—kila mumoja wao iko na sababu yenye imefanya nimuchague. Watu wenye kuzungumuziwa katika Biblia wanakuwa watu halisi kwangu kadiri ninajifunza juu yao. Nimefurahia kabisa kujifunza habari zenye kuwa katika kitabu Tuige Imani Yao, na pia katika ‘Fahirisi ya Mifano ya Kuigwa’ yenye kuwa katika buku zote mbili za kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza​—Majibu Yafanyayo Kazi.”​—Melinda.

 Shauri: Usichague tu mufano moja wa kuiga. Mutume Paulo aliwaambia Wakristo wenzake hivi: ‘Muendelee kuwaangalia wale wanaotembea katika njia inayolingana na kielelezo [ao, mufano] ambacho sisi tuliwawekea ninyi.’​—Wafilipi 3:​17.

 Ulijua? Unaweza kuwa mufano kwa mutu mwengine! Biblia inasema hivi: ‘Ukuwe kielelezo [ao, mufano] kwa waaminifu katika kusema, katika mwenendo, katika upendo, katika imani, katika usafi wa kiadili.’​—1 Timotheo 4:​12.

 “Hata kama unaweza kuwa na lazima ya kufanya sifa zako fulani zikuwe muzuri, unaweza kusaidia wengine kufanya muzuri zaidi. Wengine wanaweza kukuchunguza bila wewe kujua, na mambo yenye unasema yanaweza kubadilisha maisha ya mutu bila wewe kujua.”​—Kiana.