Ufunuo kwa Yohana 16:1-21

  • Mabakuli saba ya kasirani ya Mungu (1-21)

    • Yanamwangwa juu ya dunia (2), bahari (3), mito na chemchemi (4-7), jua (8, 9), kiti cha ufalme cha munyama wa pori (10, 11), Efrati (12-16), na hewa (17-21)

    • Vita ya Mungu kwenye Armagedoni (14, 16)

16  Na nikasikia sauti kubwa kutoka katika patakatifu+ ikiambia wale malaika saba (7): “Muende mumwange juu ya dunia yale mabakuli saba ya kasirani ya Mungu.”+  Malaika wa kwanza akaenda na kumwanga bakuli lake juu ya dunia.+ Na kidonda chenye kuumiza na chenye kuwa hatari+ kikapata watu wenye walikuwa na alama ya ule munyama wa pori+ na wenye walikuwa wanaabudu sanamu yake.+  Malaika wa pili akamwanga bakuli lake ndani ya bahari.+ Na ikakuwa damu+ kama damu ya mwanadamu mwenye alikufa, na kila kiumbe chenye uzima kikakufa,* ndiyo, vitu vyenye kuwa ndani ya bahari.+  Malaika wa tatu (3) akamwanga bakuli lake ndani ya mito na chemchemi za maji.*+ Na zikakuwa damu.+  Nikasikia malaika mwenye kuwa juu ya maji akisema: “Wewe, Mwenye uko na mwenye ulikuwa,+ Mwenye kuwa mushikamanifu,+ wewe ni mwenye haki, kwa maana umetoa hukumu hizi,+  kwa sababu walimwanga damu ya watakatifu na ya manabii,+ na umewapatia damu wakunywe;+ wanastahili jambo hilo.”+  Na nikasikia mazabahu ikisema: “Ndiyo, Yehova* Mungu, Mweza-Yote,+ hukumu zako ni za kweli na za haki.”*+  Malaika wa ine (4) akamwanga bakuli lake juu ya jua,+ na jua likapewa ruhusa ya kuunguza watu kwa moto.  Na wale watu wakaunguzwa na joto hilo kali, lakini wakatukana jina la Mungu, mwenye kuwa na mamlaka juu ya mapigo haya, na hawakutubu na kumupatia utukufu. 10  Malaika wa tano (5) akamwanga bakuli lake juu ya kiti cha ufalme cha ule munyama wa pori. Na ufalme wake ukatiwa giza,+ na wakaanza kutafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu yao, 11  lakini wakamutukana Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu yao na vidonda vyao, na hawakutubu matendo yao. 12  Malaika wa sita (6) akamwanga bakuli lake juu ya muto mukubwa Efrati,+ na maji yake yakakauka+ ili kutayarisha njia kwa ajili ya wafalme+ wenye wanatoka mashariki. 13  Na nikaona maneno machafu tatu (3) yenye yaliongozwa na roho wachafu yenye yalionekana kama vyura yakitoka katika kinywa cha ule nyoka mukubwa+ na katika kinywa cha ule munyama wa pori na katika kinywa cha ule nabii wa uongo. 14  Kwa kweli, hayo ni maneno yenye yanaongozwa na pepo wachafu na yanafanya alama,+ na yanaenda kwa wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu, ili kuwakusanya pamoja kwa ajili ya vita+ ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.+ 15  “Angalia! Ninakuja kama mwizi.+ Mwenye furaha ni ule mwenye anakaa macho+ na kuchunga nguo zake za inje, ili asitembee uchi na watu waangalie haya yake.”+ 16  Na yakawakusanya pamoja mahali kwenye kunaitwa katika Kiebrania Armagedoni.*+ 17  Malaika wa saba (7) akamwanga bakuli lake juu ya hewa. Halafu sauti kubwa ikatoka katika patakatifu+ katika kile kiti cha ufalme, ikisema: “Imefanyika!” 18  Na kukakuwa miangaza ya umeme wa radi na sauti na mingurumo ya radi, na kukatokea tetemeko kubwa la inchi lenye halifanane na tetemeko lolote lenye limekwisha kutokea tangu wanadamu wakuwe katika dunia,+ tetemeko hilo la inchi lilienea sana na lilikuwa kubwa sana. 19  Ule muji mukubwa+ ukapasuka na kuwa sehemu tatu (3), na miji ya mataifa ikaanguka; na Babiloni Mukubwa+ akakumbukwa mbele ya Mungu, ili kumupatia kikombe cha divai cha hasira ya kasirani yake kali.+ 20  Pia, kila kisiwa kikakimbia, na milima haikupatikana.+ 21  Halafu mvua kubwa ya majiwe, kila jiwe likiwa na uzito wa karibu talanta moja,* ikanyesha kutoka mbinguni juu ya watu, na watu wakamutukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya ­majiwe,+ kwa kuwa pigo hilo lilikuwa kubwa ajabu.

Maelezo ya Chini

Ao “kila nafsi ikakufa.”
Ao “mabubujiko ya maji.”
Ao “maamuzi yako ya hukumu ni ya kweli na ya haki.”
Kigiriki Har Ma·ge·donʹ, kutokana na neno la Kiebrania lenye kumaanisha “Mulima wa Megido.”
Talanta ya Kigiriki ilikuwa sawa na kilograme 20.4 (aunsi troi 654). Angalia Nyongeza B14.