Kulingana na Yohana 3:1-36

  • Yesu na Nikodemo (1-21)

    • Kuzaliwa tena (3-8)

    • Mungu alipenda ulimwengu (16)

  • Yohana anatoa ushahidi wake wa mwisho juu ya Yesu (22-30)

  • Ule mwenye anatoka juu (31-36)

3  Kulikuwa mutu mumoja kati ya Wafarisayo mwenye aliitwa Nikodemo;+ alikuwa mutawala wa Wayahudi.  Mutu huyo alikuja kwa Yesu usiku+ na kumuambia: “Rabi,+ tunajua kama umetoka kwa Mungu ukiwa mwalimu, kwa maana hakuna mutu mwenye anaweza kufanya alama+ hizi zenye unafanya kama Mungu haiko pamoja naye.”+  Yesu akamuambia: “Kwa kweli kabisa ninakuambia, kama mutu hazaliwe tena,*+ hawezi kuona Ufalme wa Mungu.”+  Nikodemo akamuuliza: “Namna gani mutu anaweza kuzaliwa tena wakati amezeeka? Je, anaweza kuingia katika tumbo la uzazi la mama yake mara ya pili na kuzaliwa tena?”  Yesu akajibu: “Kwa kweli kabisa ninakuambia, kama mutu hazaliwe kwa maji+ na roho,+ hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu.  Kile chenye kimezaliwa kwa mwili ni mwili, na kile chenye kimezaliwa kwa roho ni roho.  Usishangae kwa sababu nimekuambia: Ninyi munapaswa kuzaliwa tena.  Upepo unavuma mahali unataka, na unasikia namna unavuma, lakini haujue upepo huo unatoka wapi wala unaenda wapi. Ni vile kwa kila mutu mwenye amezaliwa kwa roho.”+  Nikodemo akamuuliza: “Mambo haya yanawezekana namna gani?” 10  Yesu akamujibu: “Wewe ni mwalimu wa Israeli, na je, haujue mambo haya? 11  Kwa kweli kabisa ninakuambia, mambo yenye tunajua tunayasema, na mambo yenye tumeona tunatoa ushahidi juu yake, lakini ninyi hamupokee ushahidi wenye tunatoa. 12  Kama nimewaambia mambo ya dunia lakini bado hamuamini, namna gani mutaamini kama ninawaambia mambo ya mbinguni? 13  Zaidi ya hayo, hakuna mutu mwenye amepanda mbinguni+ isipokuwa ule mwenye alitoka mbinguni,+ ni kusema, Mwana wa binadamu. 14  Na kama vile Musa aliinua nyoka katika jangwa,+ ni vile Mwana wa binadamu anapaswa kuinuliwa,+ 15  ili kila mutu mwenye anamuamini apate uzima wa milele.+ 16  “Kwa maana, Mungu alipenda ulimwengu sana na hivyo akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee,+ ili kila mutu mwenye anamuamini asiharibiwe lakini apate uzima wa milele.+ 17  Kwa maana Mungu hakutuma Mwana wake katika ulimwengu ili ahukumu ulimwengu, lakini ili ulimwengu uokolewe kupitia yeye.+ 18  Kila mutu mwenye anamuamini hatahukumiwa.+ Kila mutu mwenye hamuamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hana imani katika jina la Mwana muzaliwa-pekee wa Mungu.+ 19  Sasa huu ndio musingi wa hukumu: kwamba mwangaza umekuja katika ulimwengu,+ lakini watu wamependa giza kuliko mwangaza, kwa maana matendo yao yalikuwa maovu. 20  Kwa maana kila mutu mwenye anazoea kutenda mambo maovu anachukia mwangaza na hakuje kwenye mwangaza, ili matendo yake yasikaripiwe.* 21  Lakini kila mutu mwenye anafanya mambo ya kweli anakuja kwenye mwangaza,+ ili matendo yake yafunuliwe kuwa yamefanywa kupatana na Mungu.” 22  Kisha mambo haya, Yesu na wanafunzi wake wakaenda katika eneo la mashamba la Yudea, na akatumia wakati fulani pamoja nao na alikuwa anabatiza.+ 23  Lakini Yohana pia alikuwa anabatiza kule Ainoni karibu na Salimu, kwa sababu kule kulikuwa maji mengi,+ na watu walikuwa wanakuja na walikuwa wanabatizwa;+ 24  kwa maana Yohana alikuwa hajatupwa katika gereza.+ 25  Sasa wanafunzi wa Yohana walibishana na Muyahudi fulani juu ya utakaso. 26  Basi wakakuja kwa Yohana na kumuambia: “Rabi, mutu mwenye alikuwa pamoja na wewe ngambo ingine ya Yordani, mwenye ulitoa ushahidi juu yake,+ ona, anabatiza, na watu wote wanamuendea.” 27  Yohana akawaambia: “Mutu hawezi kupokea hata kitu kimoja kama tu hakupewa kitu hicho kutoka mbinguni. 28  Ninyi wenyewe munatoa ushahidi kwamba nilisema, ‘Mimi siko Kristo,+ lakini nimetumwa nimutangulie.’+ 29  Kila mutu mwenye kuwa na bibi-arusi ndiye bwana-arusi.+ Lakini wakati rafiki ya bwana-arusi anasimama na kumusikia, anafurahi sana kwa sababu ya sauti ya bwana-arusi. Basi furaha yangu imefanywa kuwa kamili. 30  Huyo anapaswa kuendelea kuongezeka, lakini mimi lazima niendelee kupunguka.” 31  Ule mwenye anatoka juu,+ iko* juu ya wengine wote. Ule mwenye anatoka katika dunia, ni wa kutoka katika dunia na anasema juu ya mambo ya dunia. Ule mwenye anatoka mbinguni, iko* juu ya wengine wote.+ 32  Anatoa ushahidi juu ya mambo yenye ameona na kusikia,+ lakini hakuna mutu mwenye anakubali ushahidi wake.+ 33  Kila mutu mwenye amekubali ushahidi wake ametia muhuri wake juu ya ushahidi huo* kwamba Mungu ni wa kweli.+ 34  Kwa maana ule mwenye Mungu ametuma anasema maneno ya Mungu,+ kwa maana Yeye anatoa roho yake kwa wingi.* 35  Baba anamupenda Mwana+ na ametia vitu vyote katika mukono wake.+ 36  Ule mwenye anamuamini Mwana iko* na uzima wa milele;+ ule mwenye hamutii Mwana hataona uzima,+ lakini kasirani kali ya Mungu inakaa juu yake.+

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “hazaliwe kutoka juu.”
Ao “yasifunuliwe.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “amehakikisha.”
Ao “hatoe roho yake kwa kipimo.”
Ao “eko.”