Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kama vile dira (boussole) yenye kutumainika, kanuni za muzuri juu ya mwenendo zitasaidia mutoto kuamua ni njia gani anapaswa kufuata

KWA AJILI YA WAZAZI

7: Kanuni za Mwenendo

7: Kanuni za Mwenendo

MAANA YAKE NINI?

Kanuni za mwenendo ni kanuni za kipekee zenye mutu anachagua kufuata. Kwa mufano, unajikaza kuwa muaminifu katika mambo yote? Kwa hiyo, unapenda bila shaka kufundisha watoto wako kanuni hizo za mwenendo.

Unapenda pia kuwafundisha kuwa ni jambo la maana kutumika kwa bidii, kuwa na usawaziko, na kufikiria wengine​—sifa zenye mutu anakomalisha muzuri zaidi wakati angali kijana.

KANUNI YA BIBLIA:Umulee [ao, zoeza] muvulana [ao, mutoto mwanaume] kulingana na njia inayomufaa; hata atakapozeeka hatageuka kando na kuiacha.’​—Methali 22:6.

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA

Katika ulimwengu wenye kuendelea katika mambo ya teknolojia, kanuni za mwenendo ni za lazima. Mama mumoja mwenye kuitwa Karyn anasema, “Mutu anaweza kuchochewa na mambo ya mubaya yenye yanaweza kupatikana wakati wowote kupitia vyombo kama vile telefone na tablette. Watoto wetu wanaweza kuwa wamekaa tu pembeni yetu wakiangalia jambo fulani lenye halifae!”

KANUNI YA BIBLIA: “Watu wakomavu . . . nguvu zao za ufahamu zimezoezwa kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa pia.”​—Waebrania 5:14.

Ni jambo la maana kufikiria wengine. Hilo linatia ndani matendo ya kawaida ya kuonyesha adabu (kama vile kusema “tafazali” na “aksanti”) na kuhangaikia wengine​—kanuni ya mwenendo yenye watu hawafuate tena zaidi, kwa sababu inaonekana kuwa watu wanahangaikia zaidi vyombo vya kielektroniki kuliko watu.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Kama vile munavyotaka watu wawatendee ninyi, muwatendee wao vivyo hivyo.’​—Luka 6:31.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

Onyesha kanuni zako za mwenendo. Kwa mufano, uchunguzi unaonyesha kuwa vijana wa miaka kati ya 13 na 19 wanaweza kabisa kujiepusha kufanya ngono mbele ya kuoa ao kuolewa ikiwa walifundishwa waziwazi kuwa kufanya hivyo ni mubaya.

SHAURI: Tumia jambo fulani lenye limefanyika hivi karibuni ili kuanzisha mazungumuzo kuhusu kanuni za mwenendo. Kwa mufano, ikiwa kuko habari juu ya mauaji, unaweza kusema: “Inahuzunisha sana kuona watu wako na hasira kubwa juu ya wengine. Unawaza watu wanafikia kuwa hivyo namna gani?”

“Ni nguvu sana watoto wachague kati ya mambo yenye kuwa sawa na mambo ya mubaya ikiwa hawajue tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na mambo ya mubaya.”​—Brandon.

Ufundishe watoto wako kufikiria wengine. Hata watoto wadogo sana wanaweza kujua kusema “tafazali” na “aksanti” na kuonyesha wengine adabu. Kitabu Parenting Without Borders kinasema, “Kadiri watoto wanaona kuwa wako sehemu ya kitu fulani chenye kufanyizwa na watu wengi zaidi​—familia, masomo, eneo​—ni hivyo wanakuwa tayari kufanya matendo ya wema yenye yanaletea pia wengine faida.”

SHAURI: Patia watoto wako kazi za nyumbani ili kuwasaidia wajifunze kuwa ni jambo la maana kutumikia wengine.

“Ikiwa watoto wetu wanazoea kufanya kazi za nyumbani leo, wakati wataishi wao wenyewe, kufanya hivyo itakuwa mwepesi. Kuhangaikia madaraka kutakuwa tayari sehemu ya maisha yao.”​—Tara.