Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulimwengu Unatufundisha Nini?

Ulimwengu Unatufundisha Nini?

Ulimwengu unaendelea kushangaza watu wenye kujifunza mambo ya nyota. Na wangali wanaendelea kutengeneza vitu vya kuwasaidia wauchunguze muzuri zaidi. Wamevumbula nini?

Ulimwengu ni wenye kupangwa muzuri. Kulingana na habari moja yenye kuwa mu gazeti Astronomy: “Magalaksi haikuwake tu ovyo-ovyo mu anga, lakini inapangwa kwa utaratibu.” Ile inawezekana namna gani? Watu wenye kujifunza mambo ya sayansi wanaamini kama kuko nguvu fulani yenye haionekane yenye inafanya magalaksi, makundi ya magalaksi, na makundi kubwa-kubwa ya magalaksi isikuwe ovyo-ovyo, lakini ikuwe inafuata mupangilio fulani.”

Namna gani ulimwengu ulifikia kupangwa muzuri vile? Unawaza kama ile mupangilio ilijitokeza tu kwa bahati? Ona maneno yenye Allan Sandage alisemaka wakati alikuwa muzima. Allan Sandage anajulikana kuwa “mumoja kati ya watu wenye walijifunzia sana mambo ya nyota mu karne ya 20,” na alikuwa anamuamini Mungu.

Alisema hivi: “Nawaza haiwezekane ile mupangilio ijitokeze yenyewe. Kunapaswa kuwa jambo yenye ilifanya kukuwe ile utaratibu.”

Namna ulimwengu umepangwa inawezesha kukuwe uzima. Fikiria ile yenye watu wenye kujifunza mambo ya sayansi wanaita nguvu zaifu (interaction faible). Ile nguvu njo inafanya jua iendelee kuwaka nguvu. Kama ile nguvu ingekuwa zaifu zaidi, jua haingekuwaka. Na kama ingekuwa nguvu zaidi, jua ingekuwa ilishakapotea tangu zamani.

Mu ulimwengu muko mambo yenye imepangwa muzuri juu uzima ukuwe, na kati ya ile mambo kuko nguvu zaifu. Mwandikaji wa mambo ya sayansi Anil Ananthaswamy anasema kama ikiwa hata jambo moja tu kati ya ile mambo ingekuwa tofauti na vile iko, “nyota, sayari, na magalaksi havingekuwa. Na haingewezekana uzima ukuwe.”

Ulimwengu uko na fasi ya muzuri sana kwa ajili ya wanadamu. Dunia iko na angahewa yenye kufaa, na kiasi yenye kufaa ya maji. Tena, iko na mwezi wenye uko na ukubwa wenye kufaa wenye unaisaidia ibakie pa nafasi yake. Gazeti National Geographic inasema kama namna dunia iko, na vitu vyenye uzima vyenye viko ndani yake, vinafanya dunia tu njo ikuwe fasi kwenye mwanadamu anaweza kuishi. *

Kulingana na mwandikaji mumoja, mufumo wetu wa jua “uko mbali na nyota zingine” mu galaksi yetu. Na ni ile njo inafanya iwezekane kukuwe uzima ku dunia. Kama tungeishi karibu na nyota zingine, ikuwe katikati ao ku mwisho-mwisho ya galaksi yetu, joto ya zile nyota ingefanya uzima usikuwe ku dunia. Lakini, kwenye dunia iko mu galaksi yetu, ni fasi kwenye inafaa kabisa juu kukuwe uzima.

Paul Davies, mwanasayansi mwenye kujua mambo mingi juu ya ulimwengu na sheria zake, alifikia kusema hivi: “Siwezi kuamini kama tuko hapa kwa bahati. Tulifanywa juu tuishi hapa.” Ni kweli kwamba Davies hafundishe kama Mungu njo aliumba ulimwengu na wanadamu. Lakini unawaza nini? Inaonekana kabisa kama ulimwengu na dunia vilifanywa mu njia yenye inawezesha kukuwe uzima. Hauone kama mambo iko vile juu kuko mwenye alivifanya?

^ fu. 8 Kusudi ya ile habari yenye kuwa mu gazeti National Geographic haikuwa kuonyesha kama Mungu njo aliumba dunia na wanadamu. Lakini ile habari ilitoa tu maelezo yenye kuonyesha kama dunia njo fasi ya muzuri kwenye mwanadamu anaweza kuishi.