Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Habari Fulani za Ulimwengu

Habari Fulani za Ulimwengu

Ekuado

Katika mwaka wa 2007, inchi ya Ekuado ilitangaza kwamba imechukua mipango ya kutumia feza ili kulinda kilometa muraba zaidi ya 10000 za musitu wa mvua wa Amazoni ambao haujalimwa kuliko kuchimba petroli ndani yake. Lakini, mipango hiyo imeachwa kwa sababu mataifa mengine hayatoe feza za kusaidia inchi hiyo kulinda mazingira. Sehemu hiyo ya musitu wa mvua wa Amazoni ni moja ya maeneo ya dunia yenye viumbe wengi.

Japani

Kitabu moja kinaonyesha kwamba ni vigumu sana kuvumbua magonjwa katika damu yoyote inayopimwa. (The Japan News) Katika mwaka wa 2013, kitabu hicho kilisema kwamba mwanaume wa zaidi ya miaka 60 aliambukizwa UKIMWI ao SIDA wakati alitiwa damu katika mishipa. Wakati damu iliyotolewa imeambukizwa na ugonjwa huo, kuna kipindi fulani ugonjwa huo hauwezi kuonekana katika damu wakati inapimwa.

Zimbabwe

Hata kama kumepita miaka zaidi ya 30 tangu waasi wa Zimbabwe waliacha kupigania kwenye mipaka yake na Mozambiki, mabomu yenye kutegwa katika udongo yanaendelea kuumiza na kuua watu. Ripoti ya Biro ya Ulimwengu ya Musalaba Mwekundu inasema kwamba “kuanzia mwaka wa 1980, watu zaidi ya 1500, wanyama zaidi 120000 wameuawa, na wakaaji zaidi ya 2000 wameumizwa na mabomu hayo kwenye mupaka wa Zimbabwe.”

Australia

Uchunguzi mumoja unaonyesha kwamba bibi na bwana wengi ambao wanatengana wanapigania wanyama wa kujifurahisha nao. Kati ya vitu ambavyo wanapigania, kuna sehemu za udongo, nyumba, feza, vitu vya kipekee, na kisha wanyama wa kujifurahisha nao.