Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | NI MUBAYA KUPATIA MUTOTO MALIPIZI?

Malipizi Yenye Kuleta Matokeo Mazuri

Malipizi Yenye Kuleta Matokeo Mazuri

BILA SHAKA, kulea watoto ni kazi ngumu. Lakini kukosa kutoa malipizi wakati ni lazima kufanya hivyo, kunafanya kazi hiyo ikuwe ngumu zaidi. Sababu gani? Kwa sababu, bila malipizi (1) watoto wanaendelea kuwa na tabia ya mubaya, na jambo hilo linachokesha sana wazazi, pia (2) wazazi wanatoa muongozo wenye kubadilika-badilika, kwa hiyo watoto hawajue wafuate muongozo gani.

Lakini, malipizi yenye kutolewa kwa upendo na kwa kiasi inaweza kuzoeza uwezo wa kufikiri wa mutoto na kumusaidia akuwe na tabia ya muzuri. Pia inasaidia watoto wajisikie salama wakati wanaendelea kukomaa na kuwa watu wazima wenye kutegemeka. Lakini unaweza kupata wapi muongozo wenye kutumainika juu ya kupatia watoto malipizi?

Kanuni za Biblia ni Zenye Faida

Wachapishaji wa gazeti hili, ni kusema, Mashahidi wa Yehova, wanaamini kama Biblia ‘ni yenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nizamu [malipizi] katika uadilifu,’ kama vile Biblia yenyewe inasema. (2 Timotheo 3:16) Biblia haiko tu kitabu cha kuonyesha namna ya kulea watoto; kanuni zake zinatoa muongozo wenye kufaa kwa ajili ya familia. Fikiria mifano fulani.

BIBLIA INASEMA HIVI: “Ujinga umefungwa moyoni mwa mutoto.”— Methali 22:15, La Sainte Bible en Swahili de la R.D. Congo.

Hata kama watoto wanaweza kuwa wenye kuhangaikia sana wengine, wako pia na muelekeo wa kufanya mambo ya ujinga. Kwa hiyo, watoto wako na lazima ya malipizi. (Methali 13:24) Kujua jambo hilo kutakusaidia wewe muzazi utimize daraka lako.

BIBLIA INASEMA HIVI: ‘Usinyime muvulana [ao mutoto] nizamu.’—Methali 23:13.

Usiogope kama ukipatia watoto wako malipizi kwa kiasi, utawaumiza ao kama watakuchukia baadaye katika maisha. Ikiwa malipizi inatolewa kwa upendo, itasaidia watoto wako wajifunze kukubali kwa unyenyekevu kurekebishwa. Watakuwa na lazima ya sifa hiyo hata wakati watakuwa watu wakubwa.—Waebrania 12:11.

BIBLIA INASEMA HIVI: ‘Lolote lile analopanda mutu, atavuna hilo pia.’—Wagalatia 6:7.

Kwa kawaida wazazi wanapenda kulinda watoto wao, na hilo ni jambo la muzuri. Lakini tena, inaomba kuwa na usawaziko. Hausaidie watoto wako wakati “unawalinda” ili wasipate matokeo ya makosa yao ao wakati unawatetea ikiwa mwalimu ao mutu mwengine mukubwa anakujulisha juu ya tabia ya mubaya ya watoto wako. Kuliko kufanya hivyo, uone kuwa watu hao wanakusaidia. Ukifanya hivyo, unafundisha watoto wako kuheshimia mamlaka; hata mamlaka yako.Wakolosai 3:20.

BIBLIA INASEMA HIVI: ‘Muvulana aliyeachiliwa atamuletea mama yake aibu [haya].’—Methali 29:15.

Ukuwe mwenye upendo, usibadilike-badilike, na usivuke mipaka

Ni kweli kwamba wazazi hawapaswe kutumia mubaya mamlaka yao, lakini hawapaswe pia kuachilia watoto wafanye kila jambo wanataka. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Watoto wenye wazazi wanaachilia wafanye kila jambo wanataka hawatambue kama ni watu wakubwa katika familia ndio wanaongoza.” (Price of Privilege) Ikiwa hautumikishe mamlaka yako, mutoto wako anaweza kuwaza kama ni yeye anaongoza. Bila shaka, atafanya maamuzi mabaya yenye yatamuumiza na yatakuumiza pia.—Methali 17:25; 29:21.

BIBLIA INASEMA HIVI: ‘Mwanaume . . . atashikamana na muke [bibi] wake, na hao wawili watakuwa mwili mumoja.’—Mathayo 19:5.

Kulingana na Biblia, mwanaume na mwanamuke wanapaswa kwanza kuoana mbele wazae watoto, na wataendelea kuishi pamoja kisha watoto kukomaa na kuondoka nyumbani. (Mathayo 19:5, 6) Hilo linamaanisha kuwa unapaswa kutia bibi ao bwana yako pa nafasi ya kwanza, na mutoto pa nafasi ya pili. Lakini ukitia mutoto pa nafasi ya kwanza, anaweza ‘kujifikiria mwenyewe zaidi kuliko ilivyo lazima kufikiri.’ (Waroma 12:3) Uhusiano wa bibi na bwana unaharibika katika familia ambamo “mutoto anatiwa pa nafasi ya kwanza.”

Musaada kwa Wazazi

Ili wewe muzazi uweze kutimiza kusudi lako, malipizi yenye unatoa inapaswa kupatana na kanuni zenye kufuata.

Ukuwe mwenye upendo. ‘Musiwe mukiwakasirisha watoto wenu, ili wasivunjike moyo.’—Wakolosai 3:21.

Usibadilike-badilike. “Acheni tu neno lenu Ndiyo limaanishe Ndiyo, Siyo yenu, Siyo.”—Mathayo 5:37.

Usivuke mipaka. “Nitakurekebisha kwa kiwango kinachofaa.”—Yeremia 30:11. *

^ fu. 21 Ili kupata habari zaidi, fungua adresi yetu ya Internete jw.org. Fungua kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > WENZI WA NDOA NA WAZAZI, na hapo utapata habari kama vile “Kuwapatia Watoto Malipizi,” “Jinsi ya Kushughulika na Mtoto Mwenye Milipuko ya Hasira,” “Uwafundishe Watoto Wako Tabia ya Muzuri,” na “Jinsi ya Kumtia Nidhamu Kijana Wako.”