Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | KULEA WATOTO

Namna ya Kusifu Watoto

Namna ya Kusifu Watoto

MAGUMU

Watu fulani wanasema kama haiwezekane kusifu mutoto wako sana. Watu wengine wanawaza kama kusifu mutoto kunaweza kumuharibisha na kumufanya ajione kuwa ana haki zote, ni kama vile wengine wako na deni lake.

Zaidi ya kuona ikiwa unamusifu mutoto wako sana, unapaswa pia kuona ni sifa ya namna gani unamupatia. Ni sifa ya namna gani itamutia moyo mutoto wako? Ni sifa ya namna gani inaweza kumuharibisha? Namna gani unaweza kusifu mutoto kwa njia yenye kuleta matokeo ya muzuri?

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Sifa zote haziko sawa. Fikiria mambo yenye kufuata.

Kusifu mutoto sana kunaweza kumuharibisha. Wazazi fulani wanapatia watoto wao sifa zenye hawastahili ili kujaribu kufanya watoto wajitumainie. Musomi David Walsh anatoa angalisho kwamba watoto “ni werevu, wanaweza kuona kama unatia chumvi na kuona kama mambo unasema hayatoke katika moyo. Wanajua kama hawakustahili [sifa] yenye walipata na wanaweza kuona kama haustahili kutumainiwa tena.” *

Ni muzuri kusifu mutoto kwa sababu ya uwezo wake. Wazia kuwa mutoto wako mwanamuke ana kipawa cha kuchora (dessiner). Kwa kawaida, unataka kumusifu juu ya jambo hilo, na hilo litamuchochea afanye uwezo wake ukuwe muzuri zaidi. Lakini kufanya hivyo kunaweza kuleta kizuizi. Kusifu mutoto wako kwa sababu tu ya kipawa kunaweza kumufanya afikiri kama ni jambo la maana kufuatia tu mambo anaweza kufanya kwa vyepesi. Anaweza hata kuogopa matatizo mapya, akiwaza kuwa atashindwa. Anaweza kuwaza, ‘Ikiwa jambo fulani linaniomba kujikaza sana, siwezi kuliweza, sababu gani nijaribu kulifanya?’

Ni muzuri zaidi kusifu mutoto kwa sababu ya bidii anafanya. Watoto wenye kusifiwa kwa sababu ya kazi yao ngumu na uvumilivu wao, kuliko kusifiwa kwa sababu tu ya vipawa vyao, wanafikia kutambua jambo hili la maana: ili kuwa na uwezo fulani, inaomba uvumilivu na bidii. Kulingana na kitabu kimoja, kujua jambo hilo kunawachochea “watumike kama vile inapaswa ili wafikie kutimiza jambo lenye wanataka. Hata kama wanashindwa kufanya jambo fulani, hawajione kuwa wa bure, lakini wanajiona kuwa wanafunzi.” (Letting Go With Love and Confidence)

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Usifu mutoto kwa sababu ya bidii yake, haiko tu kwa sababu ya kipawa chake. Kumuambia mutoto wako, “Ninaona kama unajikaza sana kuchora muzuri,” kunaweza kuwa na matokeo ya muzuri kuliko kumuambia, “Wewe uko muchoraji wa kizalikio.” Misemo hiyo yote ni yenye kusifu, lakini bila kujua musemo wa pili unaweza kuonyesha kama uwezo mbalimbali wenye mutoto wako alizaliwa nao ndio tu anaweza kufanya muzuri.

Wakati unasifu mutoto kwa sababu ya bidii alifanya, unamufundisha kama uwezo unaweza kuwa muzuri kupitia mazoezi. Mutoto wako anaweza kupambana na matatizo mapya kwa uhakika.—Kanuni ya Biblia: Methali 14:23.

Usaidie mutoto wako asivunjike moyo wakati anashindwa. Hata watu wazuri wanafanya makosa, pengine mara nyingi. (Methali 24:16) Lakini kisha kufanya kosa, hawavunjike moyo, wanajifunza kutokana na jambo hilo, na wanaendelea mbele. Namna gani unaweza kumusaidia mutoto wako akuwe na mawazo hayo ya muzuri?

Tena, umusifu kwa sababu ya bidii yake. Ona mufano huu: Fikiria unamuambia mara nyingi mutoto wako mwanamuke, “Wewe ulizaliwa na kipawa cha hesabu,” lakini kisha anashindwa mashindano (examens) ya hesabu. Anaweza kuona kama amepoteza kipawa chake, na hakuna sababu ya kujikaza ili afanye muzuri.

Hata hivyo, ikiwa unasifu mutoto kwa sababu ya bidii yake, unamusaidia akuwe na sifa ya uvumilivu. Unasaidia mutoto wako kuona kama kuteleza haiko kuanguka. Kwa hiyo, kuliko kuvunjika moyo, anaweza kujaribu njia ingine ao kufanya bidii zaidi.—Kanuni ya Biblia: Yakobo 3:2.

Umupatie mashauri yenye kujenga. Mashauri juu ya mambo yenye mutoto anapaswa kutengeneza yakitolewa kwa njia ya muzuri, yanaweza kumusaidia, kuliko kumuvunja moyo. Tena, kama unamusifu mutoto kwa ukawaida kwa njia yenye kufaa, pengine atakubali mashauri juu ya namna anaweza kufanya muzuri zaidi. Kwa hiyo, mambo yenye atatimiza yatamufurahisha na yatakufurahisha pia. —Kanuni ya Biblia: Methali 13:4.

^ fu. 8 Kutoka katika kitabu No: Why Kids—of All Ages—Need to Hear It and Ways Parents Can Say It.