Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kuwa Mutu Muzuri Kutafanya Ukuwe na Maisha ya Muzuri Wakati Wenye Kuja?

Kuwa Mutu Muzuri Kutafanya Ukuwe na Maisha ya Muzuri Wakati Wenye Kuja?

Kwa miaka mingi, watu wengi wanawaza kama kuwa mutu muzuri kutafanya wakuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja. Kwa mufano, watu wengi mu Asia wanakubaliana na hii maneno ya filozofe Confucius mwenye kujulikana sana: “Mambo yenye hauwezi penda wakufanyie na weye usiifanyie wengine.” *

JAMBO YENYE WENGI WANAAMUA KUFANYA

Watu wengi wanaendelea kuamini kama, ikiwa wanafanya mambo ya muzuri watakuwa na maisha ya muzuri wakati wenye kuja. Wanajikaza kuonyesha wengine heshima, kuwa na sifa za muzuri, wanatambua daraka yenye wako nayo mu maisha na wanaendelea kuwa na zamiri safi. Linh, mwanamuke moja mwenye kuishi mu Vietnam anasema hivi: “Niliwaza kila mara kama, ikiwa nasema kweli nitakuwa na maisha ya muzuri.”

Juu ya imani yao, watu fulani wanajikaza kufanya mambo ya muzuri. Hsu-Yun, mwanaume moja mwenye kuishi Taiwan, anasema hivi: “Nilifundishwa kama ikiwa mutu alifanya mambo ya muzuri atakuwa na furaha kisha kufa, lakini kama alifanya mambo ya mubaya atateseka.”

MATOKEO NI NINI?

Kusema kweli, wakati tunatendea wengine muzuri tunapata faida mingi. Lakini, wale wenye wanajikaza kutendea wengine muzuri, mara mingi wanafikiaka kuona kama hawatendewake muzuri sawa vile walitazamia. Shiu Ping mwanamuke moja mwenye kuishi Hong Kong, anasema hivi: “Nilijifunza kupitia mambo yenye nilijionea kama, wale wenye wanakuwaka nafanya mambo ya muzuri mara mingi hawabarikiwake. Nilifanya yangu yote ili kuhangaikia familia yangu na kufanya mambo ya muzuri. Lakini, ndoa yangu iliharibika na bwana yangu aliniacha miye na mutoto wangu mwanaume.”

Watu fulani wamefikia kuona kama, kila mara, dini haifanyake watu wakuwe wazuri. Etsuko, mwanamuke moja mwenye kuishi Japani, anasema hivi: “Nilijiunga na dini fulani na nilianza kuongoza vijana. Nilivunjika moyo sana, wakati niliona kama kulikuwa watu wenye walikuwa na matendo machafu, walipenda mashindano, na walitumia mubaya makuta ya kanisa.”

“Nilifanya yangu yote ili kuhangaikia familia yangu na kufanya mambo ya muzuri. Lakini ndoa yangu iliharibika na bwana yangu aliniacha miye na mutoto wangu mwanaume.”​—SHIU PING, HONG KONG

Watu fulani wenye wanajiingizaka sana mu mambo ya dini na wenye wanajikazaka sana kufanya mambo ya muzuri wamefikia kuvunjika moyo sana wakati mambo ya mubaya imewapata. Ile njo ilifikia Van, mwanamuke moja mwenye kuishi Vietnam. Anasema hivi: “Kila siku nilikuwa natoa matunda, maua, na chakula ku mazabahu kwa ajili ya wazazi wangu wenye walishakakufa na nilikuwa natazamia kama ningepata baraka mingi wakati wenye kuja. Hata kama nilifanya ile mambo yote ya muzuri na nilijikaza kuheshimia desturi za dini kwa miaka mingi, bwana yangu aligonjwa sana. Kisha mutoto yangu mwanamuke mwenye alikuwa na miaka 20 alikufa wakati alikuwa anasoma mu inchi ingine.”

Kama haitoshe tu kuwa mutu muzuri juu tukuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja, sasa nini njo tuko nayo lazima? Ili kupata jibu ya hii ulizo tuko na lazima ya muongozo, ni kusema, habari ya kweli yenye inaweza kujibia maulizo yetu yenye inaweza kutusaidia tukuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja. Ni wapi tunaweza kupata ile muongozo?

^ fu. 2 Ili kujua mambo mingi yenye Confucius alifundisha, ona sura ya 7, fungu ya 31-35, ya kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, yenye ilitolewa na Mashahidi wa Yehova na yenye kuwa ku www.dan124.com.