Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Nilianza Kufurahia Zaidi Kazi ya Wakolportere”

“Nilianza Kufurahia Zaidi Kazi ya Wakolportere”

Vitu vya Maana Sana vya Historia Yetu

“Nilianza Kufurahia Zaidi Kazi ya Wakolportere”

KATIKA mwaka wa 1886, vitabu mia moja vinavyoitwa L’Aurore du Millénium, buku la 1, viliondoshwa katika Maison de la Bible katika muji wa Allegheny, Pennsylvanie, Amerika, na kupelekwa Chicago, Illinois. Ndugu Charles Taze Russell alitaka kuvigawanya katika magazini ya kuuzisha vitabu. Sosaiti moja kubwa ya Amerika iliyokuwa ikigawanya vitabu vya dini ilikubali kupeleka vitabu L’Aurore du Millénium. Lakini, kisha majuma mawili, vitabu vyote vilirudishwa tena kwenye Maison de la Bible.

Inaonekana kama, mwevanjeliste mumoja aliyejulikana sana alikasirika alipoona vitabu L’Aurore du Millénium vikiwa pamoja na vitabu vyake katika maduka ya kuuzishia vitabu. Pastere huyo alisema kwa hasira kama ikiwa hawaondoe vitabu vya Russell, yeye na waevanjeliste wote wenye kujulikana sana watachukua vitabu vyao na kuvipeleka mahali pengine. Sosaiti hiyo ikalazimika kurudisha vitabu L’Aurore du Millénium. Tena, Russell alikuwa amefanya mapatano ili magazeti yatangaze vitabu vyake. Lakini, maadui wa Russell walifanya nguvu yao yote ili kuvunja mapatano hayo. Kwa hiyo basi, watu wanaotafuta kweli wangepata vitabu hivyo namna gani?

Watumishi wa wakati wote ao wakolportere, kama walivyokuwa wakiitwa, walifanya kazi kubwa sana. * Katika mwaka wa 1881, gazeti Le Phare de la Tour de Sion lilionyesha kama kulikuwa uhitaji wa wahubiri wa wakati wote 1 000 ili kugawanyia watu vichapo. Ijapokuwa wakolportere walikuwa wachache sana, wao walieneza mbegu za kweli kwa kugawanya vitabu mahali pengi na mbali. Katika mwaka wa 1897, vitabu L’Aurore du Millénium karibu milioni moja vilikuwa vimegawanywa, zaidi sana na watumishi hao wa wakati wote ao wakolportere. Wengi wao walitumia feza walizopata walipotolea watu maandikisho ya magazeti na walipoangusha vitabu ili kununua chakula na vitu vingine vya lazima walivyohitaji.

Wakolportere hao wenye bidii walikuwa watu wa namna gani? Wamoja walianza wakiwa vijana, wengine walikuwa wazee. Wengi walikuwa waseja ao bibi na bwana wasio na watoto; wale waliokuwa na watoto walikuwa wachache. Wakolportere wa kawaida walihubiri siku nzima, na wakolportere wasaidizi walihubiri saa moja ao mbili kila siku. Lakini, wengine hawakuweza kazi hiyo kwa sababu ya magonjwa na hali zingine. Kwenye mukusanyiko uliofanywa katika mwaka wa 1906, wale waliokuwa na uwezo wa kufanya kazi hiyo, waliambiwa kama ili kuwa kolportere si lazima mutu awe na “elimu nyingi, uwezo usio wa kawaida, ao ajue luga za malaika.”

Ndugu na dada hao waliokuwa tu watu wa kawaida walitimiza kazi ya ajabu katika karibu kila kontinenti. Ndugu mumoja alisema kama katika kipindi cha miaka saba alitolea watu vitabu 15 000. Alisema tena hivi: “Sikuwa kolportere ili kuwa muuzisha​-vitabu, lakini nilifanya hivyo ili kutoa ushahidi juu ya Yehova na kweli yake.” Mahali popote ambapo wakolportere walifika, walipanda mbegu za kweli na vikundi vya Wanafunzi wa Biblia vikaanza kuongezeka.

Viongozi wa dini waliwazarau wakolportere, waliwaita wauzisha-vitabu wanaotembeatembea kwa sababu wanakosa kazi ya kufanya. Munara wa Mulinzi wa 1892 ulitoa maelezo yafuatayo: “Watu wengi hawawaoni kama watumishi wa kweli wa Bwana na hawawaheshimu kama Bwana ambaye alipendezwa na unyenyekevu wao na roho yao ya kujitoa.” Bila shaka, maisha ya wakolportere hayakuwa “rahisi,” kama mumoja wao alivyosema. Ili kwenda katika maeneo yao, wakolportere walihitaji kwanza kinga na viatu vya nguvu. Wakati pesa zao zilimalizika, wakolportere waliwatolea watu vitabu ili watu wawapatie chakula. Kisha kupitisha siku nzima katika mahubiri, wahubiri hao wakiwa wamechoka lakini pia wenye furaha, walirudi ili kulala katika mahema ao katika nyumba za kulipia. Wengine walilala katika motokari ya wakolportere; motokari iliyokokotwa na punda na ambayo ilikuwa ikiwasaidia kufika katika eneo, na waliokuwa na motokari hizo hawakuhitaji kulipia nyumba. *

Kuanzia Mukusanyiko wa mwaka wa 1893 uliofanywa huko Chicago, programu ya mukusanyiko uliofanywa huko Chicago, programu ya mukusanyiko ilikuwa na hotuba za pekee kwa ajili ya wakolportere. Walizungumuzia mambo waliyojionea katika mahubiri, njia za kuhubiri, na mashauri juu ya kazi yao ya kuhubiri. Siku moja ndugu Russell aliwaambia wahubiri hao wenye bidii kama walipaswa kula vizuri asubuhi, kunywa maziwa wakati fulani mbele ya midi, na wakati wa joto kali walipaswa kutumia kreme ya baridi.

Wakati wa mikusanyiko, wakolportere waliohitaji mutu wa kuhubiri naye, walivaa utepe wa rangi ya manjano (jaune). Wakolportere wapya walihubiri na wale waliozoea kazi hiyo. Inaonekana kama mazoezi hayo yalihitajiwa. Siku moja kolportere mumoja mupya alipokuwa akimutolea mutu vitabu alimuambia hivi kwa sababu ya woga: “Hautataka vitabu hivi, sivyo?” Jambo la kufurahisha ni kwamba mutu yule alikubali vitabu na kisha muda fulani akawa dada yetu.

Ndugu mumoja aliuliza hivi, ‘Je, niendelee na biashara yangu na kutoa kila mwaka dolare 1 000 ili kutegemeza kazi ya kuhubiri, ao nianze kazi ya wakolportere?’ Aliambiwa kama Bwana angefurahia uamuzi wowote ule angechukua, lakini kutoa wakati wake kwa Bwana kwa kuwa kolportere kungemuletea baraka nyingi. Dada Mary Hinds aliona kazi ya wakolportere kuwa “njia nzuri zaidi ya kuwasaidia watu wengi.” Naye dada Alberta Crosby aliyekuwa mutu mwenye haya alisema hivi, “Nilianza kufurahia zaidi kazi ya wakolportere.”

Leo, watu wengi waliohubiriwa ao waliokuwa na wazazi wakolportere wanaendelea kufurahia uriti wao wa kiroho. Ikiwa hakuna hata mutu mumoja katika familia yako ambaye ameonja kazi ya wakolportere ao ya upainia, je unaweza kuanza ili wengine katika familia wafuate mufano wako? Ukifanya hivyo, wewe pia utaanza kufurahia zaidi na zaidi utumishi wa wakati wote kila siku.

[Maelezo ya chini]

^ Kisha 1931, “wakolportere” walianza kuitwa “mapainia.”

^ Maelezo zaidi juu ya motokari hizo yatatolewa katika gazeti litakalochapishwa karibuni.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 32]

Ili kuwa kolportere si lazima mutu awe na “elimu nyingi, uwezo usio wa kawaida, ao ajue luga za malaika”

[Picha katika ukurasa wa 31]

Kolportere Alfred Winfred Osei katika inchi ya Ghana, mwaka wa 1930

[Picha katika ukurasa wa 32]

Juu: Wakolportere Edith Keen na Gertrude Morris katika Angleterre mwaka wa 1918; chini: Stanley Cossaboom na Henry Nonkes katika Amerika, wakiwa na karto zilizo wazi zilizokuwa na vitabu walivyotolea watu.