Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Walijitoa kwa Kujipendea Katika Inchi ya Équateur

Walijitoa kwa Kujipendea Katika Inchi ya Équateur

Walijitoa kwa Kujipendea Katika Inchi ya Équateur

NDUGU mumoja kijana katika inchi ya Italie anayeitwa Bruno alihitaji kuamua. Alikuwa amemaliza masomo ya segondari akiwa na alama nyingi katika somo lao kupita wanafunzi wengine wote. Kwa hiyo, watu wa familia yake na walimu wake waliaanza kumutia moyo asome masomo ya juu. Miaka fulani iliyopita, Bruno alikuwa amejitoa kwa Yehova na alimuahidi kama atatia mapenzi yake pa nafasi ya kwanza katika maisha yake yote. Bruno alichukua uamuzi gani? Anaeleza hivi: “Nilimuambia Yehova katika sala kama nitaishi kulingana na naziri yangu ya kujitoa kwake na kumuweka pa nafasi ya kwanza katika maisha yangu. Lakini pia, katika sala hiyo nilimuambia waziwazi kama ningependa maisha yenye utendaji mbalimbali katika utumishi wake.”

Miaka michache baadaye, Bruno alihamia katika inchi ya Équateur iliyo katika Amerika ya kusini. Anasema hivi: “Yehova alijibu sala zangu katika njia nisizotazamia.” Bruno alipofika katika inchi hiyo, alishangaa kukuta vijana wengi ambao walikuwa wamehamia huko ili kumutumikia Yehova kikamili zaidi.

VIJANA ‘WANAOMUJARIBU YEHOVA’

Bruno na vijana wengine wengi duniani, wamefanya yale ambayo Yehova amesema. Yehova amesema hivi: ‘Tafazali munijaribu, kama sitawafungulia ninyi milango ya mbinguni na kuwamwangia baraka.’ (Mal. 3:10) Upendo kwa Yehova ulichochea vijana hao kuamua ‘kumujaribu Yehova’ kwa kutoa kwa kujipendea wakati, nguvu na mali zao ili kutegemeza faida za Ufalme kwa kuhamia katika inchi ambako kuna lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme.

Wahubiri hao wenye kujitolea wanapofika katika mugao wao mupya, mara moja wanaona kwamba “mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache.” (Mt. 9:37) Tuchukue mufano wa dada Jaqueline kutoka Allemagne. Kwa furaha aliandikia biro ya tawi ya Équateur hivi: “Nimetumikia Équateur kumepita sasa zaidi ya miaka miwili, na tayari ninajifunza Biblia na watu 13, na wane kati yao wanakusanyika kwa ukawaida. Jambo hilo linafurahisha sana, sivyo?” Mufano mwengine ni ule wa dada Chantal kutoka Canada anaeleza hivi: “Katika mwaka 2008, nilihamia katika eneo moja la Équateur ambako kulikuwa kutaniko moja tu. Sasa kuna makutaniko matatu katika eneo hilo na mapainia zaidi ya 30. Inapendeza sana kuona namna wapya wengi wanavyofanya maendeleo ya kiroho.” Chantal anaongeza hivi: “Hivi karibuni, nilihamia katika muji ulio kwenye metre 2 743 juu ya Milima Andes. Watu wanaoishi katika muji huo ni zaidi ya 75 000, lakini kuna tu kutaniko moja katika muji huo. Ni eneo lenye matokeo sana. Ninapata furaha nyingi kuhubiri katika eneo hilo.”

MATATIZO HAYAKOSE

Ni kweli kwamba kutumika katika inchi ya kigeni hakukose matatizo fulani. Vijana fulani walipatwa na matatizo hata mbele ya kuhama. Dada Kayla aliyetoka États-Unis anaeleza: “Maneno yasiyofaa ya ndugu fulani wanaorudi nyumbani yalinivunja moyo, hata ikiwa walikuwa na nia nzuri. Hawakuelewa kwa nini nilitaka kuhamia katika inchi ya kigeni ili kufanya kazi ya upainia. Wakati mwengine nilianza kujiuliza, ‘je, nimeamua vizuri?’” Hata hivyo, Kayla aliamua kuhama. Anaeleza hivi: “Nilisali kwa Yehova mara nyingi na kuzungumuza sana na ndugu na dada waliokomaa kiroho. Hilo lilinisaidia kuelewa kama Yehova anabariki roho ya kujitoa kwa kujipendea.”

Kujifunza luga mupya ni tatizo pia kwa wengi. Dada Siobhan kutoka Irlande anakumbuka: “Ilikuwa vigumu kwangu kuongea na watu kwa sababu ya kutokujua luga. Nilipaswa kujifunza kuwa muvumilivu, kujifunza luga kwa bidii na kujicheka nilipofanya makosa katika usemi.” Dada Anna kutoka Estonie anaongeza: “Kujifunza luga ya Kiespanyole ilikuwa vigumu sana kuliko hata kuzoea joto, vumbi na kukosa maji ya moto. Wakati fulani nilitaka kuvunjika moyo. Kwa hiyo, nilikazia uangalifu wangu juu ya maendeleo niliyofanya katika luga hiyo kuliko kufikiria tu makosa niliyofanya.”

Si rahisi kuacha familia na marafiki. Ndugu Jonathan kutoka États-Unis anasema hivi: “Nilipofika tu, nikajisikia mwenye kuvunjika moyo kwa kuachana na familia na marafiki wangu. Lakini, kujishugulisha sana na funzo langu la pekee na utumishi wangu kulinisaidia nishindane na hali hiyo. Muda kidogo baadaye, nilipata matokeo mazuri katika mahubiri na marafiki wapya katika kutaniko. Mambo hayo yalinisaidia kuwa na furaha tena.”

Tatizo lingine ni kuzoea hali ya maisha. Labda hali ya maisha katika inchi unakohamia itakuwa tofauti na ile uliyozoea. Ndugu Beau kutoka Canada anasema hivi: “Katika inchi yetu, watu hawasumbuke na mambo ya lazima sana kama vile umeme (moto), na maji katika nyumba. Lakini, katika eneo hili, umeme na maji vinakuenda mara kwa mara.” Katika inchi nyingi, umasikini unaenea sana, ni vigumu kupata motokari nzuri ili kuenda mahali fulani na watu wengi hawakusoma. Dada Ines kutoka Autriche anashinda tatizo hilo kwa kukazia uangalifu sifa nzuri za watu walio katika eneo. Yeye anasema hivi: “Watu ni wakaribishaji​-wageni sana, ni wenye fazili, tayari kusaidia na wanyenyekevu. Jambo nzuri zaidi ni kwamba wanapenda sana kujifunza mengi juu ya Mungu.”

“BARAKA HATA KUSIWE NA UHITAJI TENA”

Ni kweli kwamba vijana hao wote wanaotumika katika inchi ya Équateur wamejitolea sana, lakini, wametambua kama Yehova anatosheleza mahitaji yao “kwa wingi zaidi kupita mambo yote” waliyotazamia. (Efe. 3:20) Kwa kweli, wanaona kama wamepata “baraka hata kusiwe na uhitaji tena.” (Mal. 3:10) Wanajisikia namna gani kuhusu utumishi wao?

Ndugu Bruno anasema hivi: “Nilipofika Équateur, nilianza utumishi wangu katika eneo lenye kupendeza la Amazone. Baadaye, nilisaidia katika kazi ya ujenzi ya kupanua biro ya tawi ya Équateur. Sasa ninatumika katika Beteli. Ninakumbuka uamuzi niliochukua nilipokuwa Italie, nilimuahidi Yehova kama nitamuweka pa nafasi ya kwanza katika maisha yangu na amenisaidia kutimiza tamaa yangu ya kuwa na maisha yenye furaha na yenye utendaji mbalimbali katika utumishi wake.”

Ndugu Beau anasema hivi: “Nimekuwa rafiki sana wa Yehova kwa sababu ninaweza kutumia wakati wangu wote katika mambo ya kiroho hapa katika inchi ya Équateur. Pia, ninapata nafasi ya kutembelea sehemu zenye kupendeza katika inchi hii. Jambo ambalo nilikuwa nimetamani siku zote kupata.”

Dada Anna anasema hivi: “Sikuwazia kama inawezekana kwangu mimi, dada asiyeolewa, kufurahia maisha ya umisionere. Lakini kwa sasa, naelewa kama inawezekana. Yehova amenibariki sana kwa sababu ninafurahia sana kufanya wanafunzi, kushiriki katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme, na kuwa na marafiki wapya.”

Dada Elke anasema hivi: “Katika inchi yetu ya Autriche, nilisali kwa Yehova mara kwa mara ili nipate hata funzo moja la Biblia. Hapa katika inchi ya Équateur, ninajifunza Biblia na watu 15! Kuona uso wenye furaha wa wanafunzi wa Biblia wanaofanya maendeleo kunaniongezea furaha.”

Ndugu Joel anasema hivi: “Kufika katika inchi usiojua ili kumutumikia Yehova kunamufundisha mutu mambo mengi. Unajifunza kumutegemea Yehova zaidi, na inafurahisha kuona namna Yehova anavyobariki jitihada zako! Katika mwaka wangu wa kwanza hapa Équateur nikitokea États-Unis, hesabu ya wahubiri katika kikundi mahali ninapotumikia ilikuwa ya watu 6 sasa inakuwa ya watu 21. Kwenye Ukumbusho wa kifo cha Kristo tulikuwa watu 110.”

WEWE UTAFANYA NINI?

Ndugu na dada vijana, je, hali yenu inawaruhusu kuhamia mahali ambapo kuna lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme? Ni kweli, ili kuchukua uamuzi mukubwa kama huo inaomba kujitayarisha vizuri. Zaidi ya yote, jambo linalomuchochea mutu kuamua kuhama ni upendo mwingi kwa Yehova na kwa jirani. Ikiwa una upendo huo na unastahili, sali kwa Yehova sana kuhusu jambo hilo. Kisha, zungumuza na wazazi wako pia na wazee wa kutaniko juu ya tamaa yako. Labda kufanya hivyo kunaweza kukusaidia uelewe kama wewe pia unaweza kumutumikia Yehova katika njia hii yenye kufurahisha na kutosheleza.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 3]

“Nilisali kwa Yehova mara nyingi na kuzungumuza sana na ndugu na dada waliokomaa kiroho. Hilo lilinisaidia kuelewa kama Yehova anabariki roho ya kujitoa kwa kujipendea.”​—Kayla kutoka États-Unis

[Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 6]

Namna gani mutu anaweza kujitayarisha ili kutumikia katika inchi ya kigeni?

• Uwe na programu ya funzo la pekee kwa kawaida

• Rudilia Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 8 2011, ukurasa wa 4-6

• Zungumuza na wale ambao wamekwisha kutumikia katika inchi ya kigeni

• Tafuta kujua historia na tabia za watu wa inchi hiyo

• Ujifunze luga ya inchi hiyo

[Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 6]

Watu fulani wanaotumikia katika inchi ya kigeni wanajigaramia . . .

• kwa kufanya kazi katika inchi yao miezi michache kila mwaka

• kwa kupangisha nyumba zao ao kuachia watu biashara yao na kupokea feza kwa ukawaida kwa watu hao

• kwa kufanya kazi kupitia Internete

[Picha katika ukurasa wa 4, 5]

1 Jaqueline kutoka Allemagne

2 Bruno kutoka Italie

3 Beau kutoka Canada

4 Siobhan kutoka Irlande

5 Joel kutoka États-Unis

6 Jonathan kutoka États-Unis.

7 Anna kutoka Estonie

8 Elke kutoka Autriche

9 Chantal kutoka Canada

10 Ines kutoka Autriche