Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mahakama ya Ulaya Inaunga Mukono Haki ya Mutu ya Kukataa Kujiunga na Jeshi kwa Sababu ya Zamiri Yake

Mahakama ya Ulaya Inaunga Mukono Haki ya Mutu ya Kukataa Kujiunga na Jeshi kwa Sababu ya Zamiri Yake

Mahakama ya Ulaya Inaunga Mukono Haki ya Mutu ya Kukataa Kujiunga na Jeshi kwa Sababu ya Zamiri Yake

MASHAHIDI WA YEHOVA wanajulikana sana duniani pote kwa sababu hawakubali kujiingiza katika mambo ya politike na katika vita yoyote. Wanaamini kabisa kama wanapaswa ‘kufua panga zao ziwe majembe’ na kama hawapaswi ‘kujifunza vita tena.’ (Isaya 2:4) Hawakataze watu wengine kujiunga na jeshi. Lakini, Shahidi wa Yehova atafanya nini ikiwa inchi yake inamulazimisha kujiunga na jeshi lakini zamiri yake haimuruhusu kufanya hivyo? Kijana anayeitwa Vahan Bayatyan alipambana na tatizo hilo.

Matukio Yaliyoongoza Mupaka Kusamba Kwenye Mahakama ya Ulaya

Vahan alizaliwa huko Arménie Mwezi wa 4, 1983. Katika mwaka wa 1996, yeye na watu wengine wa familia yake walianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova, na alibatizwa alipokuwa na miaka 16. Kujifunza Biblia kulimusaidia Vahan aheshimu sana mafundisho ya Yesu Kristo, na agizo ambalo aliwapatia wanafunzi wake kwamba wasichukue silaha za vita. (Mathayo 26:52) Lakini, muda mufupi tu kisha kubatizwa, Vahan alipaswa kuchukua uamuzi muzito katika maisha yake.

Katika inchi ya Arménie, kuna sheria inayolazimisha vijana wanaume wote waingie katika jeshi wanapoeneza miaka 18. Ikiwa wanakataa, wanaweza kufungwa gerezani kwa miaka 3. Vahan alitaka kutumikia wanainchi wenzake. Lakini, hakutaka kupinga zamiri yake iliyozoezwa na Biblia. Sasa, angefanya nini?

Katika mwaka wa 2001, alipokaribia kueneza miaka 18, alianza kuandikia viongozi wa Arménie. Katika barua zake, aliwaonyesha kama zamiri yake na mambo anayoamini havimuruhusu kufanya kazi ya kijeshi. Lakini aliwaonyesha kama iko tayari kufanya kazi nyingine yoyote ambayo si ya kijeshi.

Kwa zaidi ya mwaka mumoja, Vahan aliendelea kuandikia viongozi wa Arménie ili kuwaomba waheshimu uamuzi wake wa kukataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya zamiri yake. Hata hivyo, Mwezi wa 9, 2002, Vahan alikamatwa, na kisha hapo alishitakiwa kama alikataa kutii amri ya kujiunga na jeshi. Alihukumiwa kufungwa gerezani kwa miezi 18 (mwaka 1 na miezi 6). Musimamizi wa mahakama, hakutosheka na hukumu hiyo, aliona kama mwaka 1 na nusu ilikuwa kidogo sana. Mwezi mumoja tu kisha hukumu hiyo, musimamizi huyo aliandikia mahakama yenye mamlaka zaidi, aliomba ndugu huyo apewe hukumu kali zaidi. Alisema kama uamuzi wa Vahan wa kukataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya zamiri yake na mambo ambayo anaamini ulikuwa uamuzi “hatari na usio na musingi.” Mahakama hayo yalikubali ombi la musimamizi huyo, yakaamua kumufunga Vahan gerezani kwa miezi 30 (miaka 2 na miezi 6).

Vahan alishitaki jambo hilo kwenye mahakama kubwa ya Arménie. Katika Mwezi wa 1, 2003, mahakama hiyo iliunga mukono uamuzi wa mahakama yenye mamlaka zaidi. Bila kukawia, Vahan alipelekwa kwenye gereza na kufungwa pamoja na wauaji, pamoja na watu wanaotumia dawa za kulewesha, na watu wanaolala wanawake kwa nguvu.

Namna Mambo Yalivyopitikana Kwenye Mahakama ya Ulaya

Kuanzia mwaka wa 2001, Arménie imekuwa kati ya inchi zinazofanyiza Baraza la Ulaya. Kwa hiyo, wanainchi wa Arménie wana haki ya kupeleka mashitaka yao kwenye Mahakama ya Ulaya ya Haki za Wanadamu, ikiwa hawatosheke na maamuzi yaliyochukuliwa na mahakama zote za inchi yao. Hilo ndilo jambo Vahan alichagua kufanya. Alishitaki kwenye Mahakama ya Ulaya ya Haki za Wanadamu. Katika shitaka lake, alionyesha kama kumulazimisha ajiunge na jeshi ijapokuwa zamiri yake inakataa, kunavunja Kifungu cha 9 cha Makubaliano ya Ulaya Yanayohusu Haki za Wanadamu. Aliomba haki yake ya kukataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya zamiri yake ilindwe, kupatana na mambo yanayosemwa katika kifungu hicho​—hiyo ndiyo ilikuwa mara ya kwanza mutu ajitetee kwa namna hiyo.

Tarehe 27 Mwezi wa 10, 2009, Mahakama ya Ulaya ya Haki za Wanadamu ilitoa uamuzi. Iliamua kama, uhuru wa zamiri unaozungumuziwa katika Kifungu cha 9 cha Makubaliano ya Ulaya, haulinde haki ya wale wanaokataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya zamiri yao.

Wakati huo, Vahan alikuwa amekwisha kuachiliwa, alikuwa amekwisha kuoa, na alikuwa na mutoto mudogo. Alivunjika moyo sana kwa sababu ya uamuzi huo. Kwa hiyo, alipaswa kuamua ikiwa ataachia hapo ao kushitaki tena kwenye Baraza Kubwa la Mahakama ya Ulaya ya Haki za Wanadamu. Aliamua kushitaki tena kwenye Baraza Kubwa la Mahakama ya Ulaya. Kwa sababu Baraza Kubwa halikubali kushugulikia mashitaka yote, Vahan alifurahi sana lilipokubali kuchunguza shitaka lake.

Mwishowe, tarehe 7 Mwezi wa 7, 2011, katika muji wa Strasbourg, huko France, Baraza Kubwa la Mahakama ya Ulaya ya Haki za Wanadamu lilitoa uamuzi wake. Kati ya waamuzi 17, waamuzi 16 walikubali kama Arménie ilivunja haki ya Vahan Bayatyan ya kuwa na uhuru wa zamiri, ilipomuhukumu na kumufunga gerezani kwa sababu alikataa kujiunga na jeshi. Muamuzi mumoja tu aliyekuwa wa huko Arménie, ndiye hakukubaliana na wenzake.

Sababu gani uamuzi huo ulikuwa wa lazima? Kwa sababu hiyo ndiyo ilikuwa mara ya kwanza Mahakama ya Ulaya ya Haki za Wanadamu inalinda haki ya mutu ya kukataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya zamiri yake, kupatana na kifungu cha 9 cha Makubaliano ya Ulaya Yanayohusu Haki za Wanadamu. Mahakama iliona kama, katika inchi ya kidemokrasia, kumufunga mutu anayekataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya zamiri yake, ni kuvunja haki zake za musingi.

Juu ya Mashahidi wa Yehova wanaokataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya zamiri yao, Mahakama ilisema maneno yanayofuata: “Kwa hiyo, Mahakama haina sababu yoyote ya kushakia sababu iliyomufanya mutu huyo akatae kujiunga na jeshi. Alifanya hivyo kwa sababu kujiunga na jeshi kunapingana kabisa na mambo anayoamini ambayo anashikilia sana.”

Matokeo ya Uamuzi huo

Katika miaka 20 iliyopita, Mashahidi wa Yehova zaidi ya 450 wa huko Arménie, ambao walikataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya zamiri yao wamehukumiwa. Kwa mufano, wakati habari hii ilikuwa inatayarishwa, vijana wanaume 58 katika inchi hiyo walikuwa katika gereza kwa sababu zamiri yao na mambo wanayoamini havikuwaruhusu kujiunga na jeshi. Vijana 5 kati yao walitiwa katika gereza kisha tu uamuzi wa Baraza Kubwa kuhusu kusamba kati ya Bayatyan na Arménie. * Kijana mumoja kati ya vijana hao alimuandikia musimamizi wa mahakama ya eneo lao ili kumuomba amalize mashitaka juu yake, lakini musimamizi huyo alikataa ombi hilo. Musimamizi huyo alimujibu hivi katika barua yake: “Uamuzi uliotolewa na Mahakama ya Ulaya tarehe 7 Mwezi wa 7, 2011 kuhusu kusamba kati ya Bayatyan na Arménie, hauhusu hali yako kwa sababu ni wazi kwamba hali yako haifanane na yake.”

Sababu gani musimamizi huyo alijibu hivyo? Wakati Vahan Bayatyan alihukumiwa, sheria ya Arménie ilikuwa haijaonyesha kazi nyingine ambayo mutu anaweza kufanya ikiwa anakataa kujiunga na jeshi. Sasa katika serikali ao guvernema ya Arménie kumekuwa sheria hiyo. Lakini, kazi hiyo inaongozwa na jeshi. Kwa hiyo, wengi kati ya wale wanaokataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya zamiri yao hawakubali pia kazi hiyo.

Vahan Bayatyan anafurahia sana uamuzi muzuri uliofanywa kwa faida yake. Kwa sababu ya uamuzi huo, sasa inchi ya Arménie inalazimishwa kuacha kuhukumu na kufunga watu ambao wanakataa kujiunga na jeshi kwa sababu ya mambo wanayoamini.

Kusudi la Mashahidi wa Yehova si kugeuza sheria za inchi ambamo wanaishi. Hata hivyo, wanatumia sheria fulani za inchi yao ili kulinda haki zao, kama vile kijana Vahan Bayatyan alivyofanya. Sababu gani wanafanya hivyo? Wanafanya hivyo ili waendelee kuishi kwa amani na kutii amri za Yesu Kristo, Kiongozi wao.

[Maelezo ya chini]

^ Vijana wawili kati yao walitiwa katika gereza tarehe 7 Mwezi wa 7, 2011, ileile siku ambayo Mahakama ya Ulaya ya Haki za Wanadamu ilitoa uamuzi.

[Picha katika ukurasa wa 30]

Vahan Bayatyan mbele ya Gereza Nubarashen huko Arménie

[Picha katika ukurasa wa 30]

Bayatyan na washauri wake wa mambo ya sheria kwenye Mahakama ya Ulaya ya Haki za Wanadamu, tarehe 24 Mwezi wa 11, 2010

[Picha katika ukurasa wa 31]

Bayatyan, bibi yake Tsovinar, na Vahe mutoto wao