Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Je, zambi zetu zinaweza kusamehewa?

Kukubaliwa na Mungu si jambo ngumu sana

Kulingana na Biblia, wanadamu wote ni wenye zambi. Tuliriti muelekeo wa kufanya zambi kutoka kwa Adamu, mutu wa kwanza. Kwa hiyo, wakati fulani tunafanya mambo mabaya ambayo tunaweza kusikitikia baadaye. Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, alitulipia deni la zambi kwa kufa kwa ajili yetu. Zabihu yake ya ukombozi iliwezesha tusamehewe zambi zetu. Ni zawadi kutoka kwa Mungu.​—Soma Waroma 3:23, 24.

Watu fulani wamefanya zambi nzito na wanajiuliza ikiwa Mungu anaweza kusamehe zambi zao. Jambo la kufurahisha ni kwamba Neno la Mungu linasema hivi: ‘Damu ya Yesu Mwana wake inatusafisha kutoka katika zambi yote.’ (1 Yohana 1:7) Yehova anasamehe bila kulazimishwa hata zambi nzito ikiwa tuna mutazamo unaofaa na ikiwa tunatubu.​—Soma Isaya 1:18.

Tunapaswa kufanya nini ili tusamehewe?

Ikiwa tunataka Yehova Mungu atusamehe, tunahitaji kujifunza juu yake, ni kusema, kuelewa njia zake, mashauri yake, na mambo ambayo anataka tufanye. (Yohana 17:3) Yehova anasamehe kabisa wale wanaotubu makosa yao na kujikaza kubadilika.​—Soma Matendo 3:19.

Kukubaliwa na Mungu si jambo ngumu sana kwetu. Yehova anaelewa uzaifu wetu. Yeye ni mwema na mwenye rehema. Fazili zake zenye upendo zinakuchochea utake kujifunza mengi juu ya namna unaweza kumupendeza, sivyo?​—Soma Zaburi 103:13, 14.