Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 KICHWA | MUNGU ANAKUONA

Mungu Anakuelewa

Mungu Anakuelewa

“Ee Yehova, umenichunguza kabisa, nawe unanijua.” —ZABURI 139:1.

““Macho yako yalikiona kiini-tete changu.” —ZABURI 139:16

SABABU INAYOFANYA WATU FULANI WAWE NA MASHAKA: Watu fulani wanafikiri kwamba Mungu anaona wanadamu kuwa tu wenye zambi, ni kusema, wasiokuwa safi na wasiostahili kuhangaikiwa naye. Kendra, ambaye alisumbuliwa na hali ya kuvunjika moyo, alijisikia kuwa mwenye makosa sana kwa sababu hakuweza kutimiza kabisa mambo Mungu anataka. Kwa hiyo, alisema hivi: “Niliacha kusali.”

MAMBO NENO LA MUNGU LINAFUNDISHA: Yehova hakazie uangalifu makosa yako na anaelewa namna uko kabisa. Biblia inasema hivi: “Analijua vema umbo letu, akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.” Zaidi ya hilo, hatutendee ‘kulingana na zambi zetu’ lakini anatusamehe kwa rehema wakati tunatubu.—Zaburi 103:10, 14.

Fikiria Daudi, mufalme wa Israeli aliyetajwa katika habari ya kwanza. Katika sala, Daudi alimuambia Mungu hivi: “Macho yako yalikiona kiini-tete changu, na katika kitabu chako sehemu zake zote zilikuwa zimeandikwa . . . Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu.” (Zaburi 139:16, 23) Kwa kweli, Daudi alikuwa na uhakika kwamba hata ikiwa alifanya zambi, hata zambi nzito wakati fulani, Yehova angetambua moyo wake wenye kutubu.

Yehova anakuelewa vizuri kuliko namna mwanadamu yeyote anakuelewa. Biblia inasema hivi: ‘Mwanadamu anaona kile kinachoonekana kwa macho, lakini Yehova anaona jinsi moyo ulivyo.’ (1 Samweli 16:7) Mungu anajua ni nini inayokufanya utende kwa njia fulani, ni kusema, anajua namna mambo kama vile hali uliyoriti, namna ulikomaa, mazingira yako, na tabia yako, yanakufanya uwe namna uko. Anaona na anapendezwa na namna unajikaza kuwa, hata ikiwa unafanya makosa.

Hata hivyo, namna gani Mungu anatumia uelewaji wake mwingi wa ‘namna uko kabisa’ ili kukufariji?