Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | NAMNA YA KUPIGANISHA MAHANGAIKO

Kila Mahali Kuna Mahangaiko!

Kila Mahali Kuna Mahangaiko!

“Nilienda kununua chakula lakini nilikuta biskuti tu, na bei yake ilikuwa imeongezeka sana! Siku yenye ilifuata, maduka yote hayakuwa na chakula.”—Paul, inchi ya Zimbabwe.

“Bwana yangu aliniikalisha na akaniambia atatuacha.Namna gani ningevumilia hali hiyo? Watoto wangu wangekuwa namna gani?”—Janet, inchi ya Amerika.

Wakati ninasikia kelele ya kuonya watu juu ya hatari, ninakimbia ili kujificha na ninalala chini wakati bombe zinapigwa. Saa nyingi kisha hapo, mikono yangu inaendelea kutetemeka.”—Alona, inchi ya Israeli.

Tunaishi nyakati za mahangaiko, ‘nyakati za hatari zilizo ngumu kushugulika nazo.’ (2 Timotheo 3:1) Watu wengi wanasumbuka kwa sababu ya matatizo ya feza, kuvunjika kwa familia, vita, magonjwa hatari, na misiba ya asili ao misiba yenye kuletwa na wanadamu. Zaidi ya hayo, kila mutu iko na mahangaiko yake mwenyewe. Kwa mufano, mutu anaweza kujiuliza hivi: ‘Kivimba chenye nilivumbua kwenye mwili wangu kitageuka kuwa kansere?’ ‘Watoto wa watoto wangu watakomalia katika dunia ya namna gani?’

Mahangaiko yote haiko mubaya. Kwa kawaida tunakuwa na mahangaiko mbele ya kufanya mashindano, mbele ya kufanya onyesho, ao mbele ya kuulizwa maulizo na mutu mwenye atatupatia kazi. Na woga wenye kufaa wa hatari unatusaidia tusipatwe na mambo mabaya. Lakini mahangaiko yenye kupita mipaka ao ya kila mara yanaleta hatari. Uchunguzi mbalimbali wa hivi karibuni wenye ulifanywa juu ya watu wazima 68 000 ulionyesha kama hata mahangaiko madogo ya kila mara yanaweza kufanya mutu akufe mbio. Kwa hiyo, Yesu alikuwa na sababu ya muzuri ya kuuliza hivi: ‘Ni nani kati yenu kwa kuhangaika anaweza kuongeza kipimo cha mukono mumoja kwenye uhai wake?’ Kwa kweli, mahangaiko hayarefushe maisha ya mutu. Ndiyo maana Yesu alitoa shauri hili: ‘Muache kuhangaika.’ (Mathayo 6:25, 27) Lakini, namna gani mutu anaweza kuacha kuhangaika?

Mutu anaweza kuacha kuhangaika ikiwa anatenda kwa hekima, anakuwa na imani ya kweli kwa Mungu, na anakuwa na tumaini la kweli kwa ajili ya wakati unaokuja. Hata kama leo hatupambane na hali ngumu, tunaweza kupambana nazo wakati unaokuja. Kwa hiyo, tuone namna kufanya mambo hayo kulisaidia Paul, Janet, na Alona wapiganishe mahangaiko yao.