Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | WATU WALIOKUFA—WANAWEZA KUISHI TENA?

Kutakuwa Ufufuo—Namna Gani Unaweza Kuwa Hakika?

Kutakuwa Ufufuo—Namna Gani Unaweza Kuwa Hakika?

Ni kukosa akili kuwaza kama watu waliokufa wataishi tena? Mutume Paulo hakuwaza vile. Roho ya Mungu ilimuongoza kuandika hivi: ‘Ikiwa ni katika maisha haya tu tumemutumaini Kristo, sisi ndio wa kusikitikiwa zaidi kati ya watu wote. Hata hivyo, sasa Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo.’ (1 Wakorintho 15:19, 20) Paulo aliona ufufuo kuwa jambo la hakika. Alipata uhakika huo kwa sababu ya ufufuo wa Yesu mwenyewe. * (Matendo 17:31) Ndiyo maana Paulo alimuita Yesu “matunda ya kwanza” kwa sababu Yesu alikuwa wa kwanza kufufuliwa ili kuishi milele. Kama Yesu alikuwa wa kwanza, ni kusema kuko wengine.

Ayubu alimuambia Mungu hivi: “Utaitamani sana kazi ya mikono yako.”—Ayubu 14:14, 15

Kuko jambo lingine lenye linaweza kukusaidia ukuwe hakika kama kutakuwa ufufuo. Yehova ni Mungu anayesema kweli. ‘Mungu, . . . hawezi kusema uwongo.’ (Tito 1:2) Yehova hajasema uwongo hata siku moja na hakuna siku atasema uwongo. Anaweza kuahidi ufufuo, kuonyesha kama anaweza kufufua watu, na kisha akose kutimiza ahadi hiyo? Jambo hilo haliwezekane kabisa!

Sababu gani Yehova amepanga kuwe ufufuo wakati unaokuja? Kwa sababu ya upendo wake. Ayubu aliuliza hivi: ‘Mutu akikufa, anaweza kuishi tena?’ Alijibu hivi: “Wewe utaita, na mimi mwenyewe nitakujibu. Kwa kuwa utaitamani sana kazi ya mikono yako.” (Ayubu 14:14, 15) Ayubu alikuwa hakika kama Baba yake wa mbinguni atatamani kumufufua. Mungu amebadilika? “Mimi ni Yehova; sikubadilika.” (Malaki 3:6) Mungu angali anatamani kufufua wafu, wakiwa na furaha na afya ya muzuri kabisa. Kila muzazi mwenye upendo anaweza kutamani kufanya hivyo kisha mutoto wake kufa. Lakini tofauti ni kwamba Mungu yeye iko na uwezo wa kufanya jambo lenye anataka.—Zaburi 135:6.

Kifo ni jambo mubaya sana, lakini Mungu anatoa tumaini la muzuri

Yehova atamupatia Mwana wake uwezo wa kuletea furaha kubwa wale wote wenye wamehuzunika sana kwa sababu ya kufiwa na watu wenye walikuwa wanapenda. Na Yesu anajisikia namna gani juu ya ufufuo? Mbele ya kumufufua Lazaro, Yesu aliona huzuni yenye dada za Lazaro na marafiki wake walikuwa nayo, naye “akatokwa na machozi.” (Yohana 11:35) Wakati mwengine, Yesu alikutana na mujane wa Naini, mwenye alifiwa na mutoto mumoja tu ambaye alikuwa naye. Yesu ‘akamusikitikia, akamuambia: Acha kulia.’ Na mara moja akafufua mutoto wake. (Luka 7:13) Kwa hiyo, Yesu anachukia sana kuona huzuni na kifo. Atafurahi sana wakati atageuza huzuni kuwa furaha katika dunia yote!

Umekwisha kupoteza mutu fulani katika kifo? Unaweza kuwaza kama kisha kifo, hakuna tumaini lolote. Lakini kuko tumaini, tumaini hilo ni ufufuo wenye Mungu atafanya kupitia Mwana wake. Ukumbuke kama Mungu anapenda uone ufufuo huo. Anapenda ukuwe hapo ili uwakumbatie tena watu wenye ulikuwa unapenda. Wazia unaishi milele na milele pamoja na watu wenye unapenda bila kuachana nao tena!

Lionel, mwenye tulitaja katika habari ya kwanza, anasema hivi: “Mwishowe, nilijifunza juu ya ufufuo. Mwanzoni, ilikuwa vigumu kuamini, na sikuaminia mutu mwenye aliniambia juu ya jambo hilo. Lakini nilitafuta mimi mwenyewe katika Biblia na nikaona kama ni kweli! Ninangojea kwa hamu kuona tena baba ya mama yangu.”

Unapenda kujua mengi zaidi? Mashahidi wa Yehova watafurahia kukuonyesha katika Biblia yako mwenyewe sababu gani wanaamini kama kutakuwa ufufuo wakati unaokuja. *

^ fu. 3 Ili kupata uhakika kama Yesu alifufuliwa, soma kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? ukurasa wa 78 mupaka 86. Kitabu hicho kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova.

^ fu. 9 Tafazali, soma sura ya 7 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova.