Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | MASHAHIDI WA YEHOVA NI NANI?

Sababu Gani Tunahubiri?

Sababu Gani Tunahubiri?

Pengine kitu chenye kutufanya tukuwe tofauti zaidi na watu wengine ni kazi yetu kubwa ya kuhubiri. Tunahubiri nyumba kwa nyumba, nafasi zenye kuwa na watu wengi, na kila nafasi watu wanapatikana. Sababu gani tunafanya hivyo?

Mashahidi wa Yehova wanahubiri ili kusifu Mungu na kujulisha wengine jina lake. (Waebrania 13:15) Tena, tunapenda kutii Kristo Yesu mwenye aliamuru hivi: ‘Muende mukafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, . . . na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.’—Mathayo 28:19, 20.

Zaidi ya hilo, tunapenda majirani wetu. (Mathayo 22:39) Ni kweli, tunatambua kama watu wengi wako na dini zao na kama haiko kila mutu atakubali ujumbe wetu. Lakini, tunaona kama mafundisho ya Biblia ni yenye kuokoa uzima. Ndiyo sababu tunaendelea “bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema juu ya Kristo Yesu,” kama vile Wakristo wa kwanza walifanya.—Matendo 5:41, 42.

Antonio Cova Maduro, mutu mwenye kujifunza namna watu wanapangwa, aliandika juu ya “bidii Mashahidi wa Yehova wanaonyesha na magumu wanapata, na kufikia hata kuchoka sana. . . , ili maandishi matakatifu yafike katika maeneo ya mbali zaidi ya dunia.”—Gazeti El Universal, Venezuela

Watu wengi wenye kusoma vichapo vyetu hawako Mashahidi wa Yehova. Na mamilioni ya watu wenye tunafundisha Biblia, wako na dini zao. Lakini, wanafurahi kuona Mashahidi wa Yehova wanawatembelea.

Pengine unaweza kuwa na maulizo mengine juu ya Mashahidi wa Yehova. Tunakutia moyo utafute majibu kwa:

  • Kuuliza Shahidi mumoja wa Yehova.

  • Kufungua adresi yetu ya Internete www.dan124.com.

  • Kufika kwenye mikutano, yetu.Hatuombe malipo na watu wote wanaweza kuingia.