Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUENDELEE KUKESHA!

Dunia Inaendelea Kuharibiwa—Biblia Inasema Nini?

Dunia Inaendelea Kuharibiwa—Biblia Inasema Nini?

 “Hivi karibuni, kunaweza kutokea misiba ya hali ya hewa. Maji itafunika miji mikubwa. Kutakuwa kivukutu sana. Kutatokea upepo mukali sana. Maji itakosekana fasi mingi. Mamilioni ya aina za mimea na wanyama fulani zitapotea. Haiko mambo ya kuwazia, na sitilie chumvi. Sayansi inaonyesha kama mambo itakuwa vile ikiwa hatufanye jambo fulani.”—Hotuba ya António Guterres, sekretere mukubwa wa Umoja wa Mataifa, kuhusu ripoti ya Kikundi ya Serikali Mbalimbali ya Wachunguzi wa Hali ya Hewa yenye ilitolewa tarehe 4, Mwezi wa 4, 2022.

 “Wanasayansi wanasema kama mu miaka yenye iko nakuya karibu parke zote 423 [mu Amerika] zitaharibiwa na mabadiliko ya hali ya hewa juu zinaweza kuharibika zaidi sana wakati kunakuwa kivukutu sana. Mambo ya mubaya yenye inaweza kutokea inafanana na misiba yenye Biblia inazungumuzia: moto na garika, kuyeyuka kwa barafu (glace), kupanda kwa maji ya bahari na kivukutu.”—“Hali ya Mubaya ya Mafuriko mu Yellowstone, Alama ya Magumu Yenye Itatokea,” The New York Times, ya tarehe 15, Mwezi wa 6, 2022.

 Matatizo ya hali ya hewa itaishaka? Kama ni vile, nani njo ataimalizaka? Ona mambo yenye Biblia inasema.

Biblia ilisemaka zamani kama wanadamu wataharibu dunia

 Biblia inasema kama Mungu ‘ataharibu wale wenye wanaharibu dunia.’ (Ufunuo 11:18) Hii andiko inatufundisha mambo tatu:

  1.  1. Mambo yenye wanadamu wanafanya itaharibu sana dunia.

  2.  2. Dunia haitaendelea kuharibiwa.

  3.  3. Mungu tu njo atamaliza matatizo ya hali ya hewa, hapana wanadamu.

Tuko hakika kama dunia itakuwa muzuri

 Biblia inasema kama “dunia inadumu milele.” (Muhubiri 1:4) Itaikaliwa milele.

  •   “Wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.”​—Zaburi 37:29.

 Dunia yetu itarudia mu hali ya muzuri kabisa.

  •   “Jangwa na inchi yenye kukauka vitafurahi, jangwa tambarare litashangilia na kutoa maua kama zafarani.”​—Isaya 35:1.