MUENDELEE KUKESHA!
Mukubwa Fulani wa Mambo ya Afya Anaonya Kuhusu Hatari ya Site za Kupashana Habari kwa Vijana—Biblia Inasema Nini?
Tarehe 23, Mwezi wa 5, 2023, mukubwa fulani wa mambo ya afya katika Amerika alionya watu kama site za kupashana habari ziko na matokeo ya mubaya juu ya vijana wengi.
“Hata kama site za kupashana habari ziko na faida kwa watoto na vijana fulani, kuko ushuhuda wenye kuonyesha kama site za kupashana habari zinaweza kuwa hatari kwa afya ya kiakili na hali ya muzuri ya watoto na vijana.”—Social Media and Youth Mental Health: The U.S. Surgeon General’s Advisory, 2023.
Ile onyo ilizungumuzia uchunguzi wenye unaonyesha juu ya nini tunapswa kuchukua ile jambo kwa uzito.
Vijana wenye kuwa kati ya miaka 12 na 15 “wenye wanapitisha zaidi ya saa 3 kila siku ku site za kupashana habari, wako mu hatari zaidi ya kuwa na matatizo ya kiakili kutia ndani kushuka moyo na kuwa na mahangaiko.”
Kati ya vijana wenye kuwa na miaka 14, “kutumia sana site za kupashana habari kunaweza kufanya wakuwe na matatizo ya kupata usingizi, kusumbuliwa ku enternete, kujiona kuwa hawavutie, kujiona kuwa hawako wa maana, na uwezekano mukubwa wa kushuka moyo, zaidi sana vijana wanamuke kuliko vijana wanaume.”
Namna gani wazazi wanaweza kulinda watoto wao na ile hatari? Biblia inatoa mashauri yenye inaweza kusaidia.
Mambo yenye wazazi wanaweza kufanya
Ushugulikie mambo. Ukiwa muzazi, fikiria hatari za kutumia site za kupashana habari na uamue ikiwa mutoto wako atazitumia ao hapana.
Kanuni ya Biblia: “Zoeza mutoto mwanaume katika njia yenye anapaswa kufuata.”—Mezali 22:6, maelezo ya chini.
Ili kujua mambo mingi zaidi, soma habari “Je, Mtoto Wangu Atumie Mitandao ya Kijamii?”
Kama unaruhusu mutoto wako atumie site za kupashana habari, ukuwe macho juu ya hatari zenye zinaweza kutokea na ujue mambo yenye mutoto wako anafanyaka ku zile site. Namna gani?
Linda mutoto wako kutokana na mambo yenye inaweza kumuumiza. Zoeza mutoto wako ili ajue namna ya kutambua na kuepuka mambo yenye kuumiza.
Kanuni ya Biblia: “Uasherati na kila namna ya ukosefu wa usafi ao pupa visitajwe hata kidogo katikati yenu, . . . “wala mwenendo wa haya wala maneno ya kipumbavu wala mizaha michafu.”—Waefeso 5:3, 4.
Ili kuona namna unaweza kufanya vile, soma habari “Mfundishe Kijana Wako Kutumia Mitandao ya Kijamii kwa Njia Salama.”
Tia mipaka. Kwa mufano, tia mipaka kuhusu ni wakati gani na kwa muda gani mutoto wako atatumia site za kupashana habari.
Kanuni ya Biblia: “muendelee kuwa waangalifu sana ili namna munatembea [ikuwe] . . . kama watu wenye hekima, mukitumia muzuri zaidi wakati wenu.”—Waefeso 5:15, 16.
Tumia video ya muchoro kwenye ubao Tumia kwa Hekima Site za Enternete za Kupashana Habari ili kusaidia mutoto wako aelewe juu ya nini mipaka ni ya lazima.