Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Programu za Usomaji wa Biblia

Programu za Usomaji wa Biblia

Biblia iko na hekima ya muzuri sana yenye inaweza kutusaidia mu maisha. Kama unazoea kuisoma na kufikiri sana juu ya mambo yenye unasoma, na kama unatumikisha mambo yenye unajifunza, “njia yako itakuwa na matokeo ya muzuri.” (Yoshua 1:8; Zaburi 1:1-3) Pia, utamujua Mungu na Mwana wake, Yesu. Na ule ujuzi unaweza kukusaidia ufikie kuokolewa.​—Yohana 17:3.

Unapaswa kusoma Biblia kwa kufuata utaratibu gani? Unaweza kujichagulia utaratibu wenye utafuata. Hii programu ya usomaji wa Biblia inakusaidia usome vitabu vya Biblia kulingana na namna vinafuatana ao kwa kuchagua habari kulingana na vichwa vyenye vimeonyeshwa. Kwa mufano, unaweza kusoma habari fulani zenye umechagua ili kujua historia yenye kuonyesha namna Mungu alitendea Waisraeli zamani. Unaweza kusoma sehemu zingine ili kujua namna kutaniko la Kikristo lilianza na namna liliendelea. Kama unasoma sehemu moja yenye kuwa na sura mbalimbali, utamaliza kusoma Biblia yote mu mwaka moja.

Ikuwe uko unatafuta programu ya kusoma Biblia kila siku ao ya kusoma Biblia kwa mwaka moja, ao programu ya usomaji wa Biblia kwa ajili ya watu wenye wanaanza kusoma Biblia, hii programu itakusaidia. Chukua hii programu ya usomaji wa Biblia yenye inaweza kuchapishwa, na uanze kusoma leo.