Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

23

Waisraeli Wanamutolea Yehova Ahadi

Waisraeli Wanamutolea Yehova Ahadi

Karibu miezi mbili kisha Waisraeli kutoka Misri, walifika ku Mulima Sinai na kutia kambi pale. Yehova akaita Musa, na Musa akapanda ku mulima. Kisha Yehova akamuambia: ‘Ni mimi niliokoa Waisraeli. Kama wananitii na kufuata sheria zangu, watakuwa watu wangu wa pekee.’ Musa akashuka kutoka ku mulima na kuambia Waisraeli maneno yenye Yehova alisema. Walimujibia namna gani? Walisema: ‘Tutafanya kila kitu chenye Yehova anatuambia tufanye.’

Musa akapanda tena ku mulima. Kule ku mulima, Yehova akamuambia: ‘Kisha siku tatu, nitazungumuza na wewe. Uambie watu wasijaribu kupanda ku Mulima Sinai.’ Musa akashuka kutoka ku mulima na akaambia Waisraeli wajitayarishe kusikiliza maneno yenye Yehova atasema.

Kisha siku tatu, Waisraeli waliona miangaza ya radi na mawingu ya mweusi sana ku mulima. Tena, walisikia sauti kubwa sana ya mingurumo ya radi na sauti ya pembe. Kisha Yehova akashuka kutoka ku mulima katika moto. Waisraeli waliogopa sana na kutetemeka. Mulima wote ulitetemeka sana na moshi iliufunika. Sauti ya pembe iliendelea kuongezeka. Kisha Mungu akasema: ‘Mimi ni Yehova. Hamupaswe kuabudu miungu ingine.’

Musa akapanda tena ku mulima, na Yehova akamupatia sheria. Zile sheria zilionyesha vile watu walipaswa kumuabudu, na vile walipaswa kutenda. Musa akaandika zile sheria kisha akazisomea Waisraeli. Wakatoa ahadi hii: ‘Tutafanya mambo yote yenye Yehova anatuambia tufanye.’ Waisraeli walimutolea Mungu ahadi. Sasa, wangeitimiza?

“Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.”​—Matayo 22:37