Ona video zinazopatikana

Ni Nani Aliyeanzisha Dini ya Mashahidi wa Yehova?

Ni Nani Aliyeanzisha Dini ya Mashahidi wa Yehova?

 Mashahidi wa Yehova wa siku hizi walianza mwishoni mwa miaka ya 1800. Wakati huo, kikundi kidogo cha wanafunzi wa Biblia walioishi karibu na muji wa Pittsburgh, Pennsylvanie, katika États-Unis, walianza kuchunguza Biblia kwa undani. Walilinganisha mafundisho ya makanisa na mambo ambayo Biblia inafundisha kabisa. Walianza kuchapisha mambo waliyojifunza katika vitabu, magazeti, na walichapisha gazeti linaloitwa sasa Munara wa Mulinzi—Unaotangaza Ufalme wa Yehova.

 Mwanaume mumoja anayeitwa Charles Taze Russell alikuwa katika kikundi hicho cha wanafunzi hao wenye bidii wa Biblia. Alisimamia kazi ya kuhubiri wakati huo na alikuwa wa kwanza kusimamia uchapishaji wa gazeti Munara wa Mulinzi, lakini si yeye aliyeanzisha dini ya Mashahidi wa Yehova. Muradi wa Russell na wenzake, ulikuwa kueneza mafundisho ya Yesu Kristo na kufuata mufano wa Kutaniko la Kikristo la wakati wa mitume. Yesu aliyeanzisha Ukristo ndiye aliyeanzisha dini yetu.—Wakolosai 1:18-20.