Ona video zinazopatikana

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Pasaka?

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Pasaka?

Mawazo ya watu wengi

 Uongo: Mashahidi wa Yehova hawasherehekeake Pasaka juu hawako Wakristo.

 Ukweli: Tunaamini kama Yesu Kristo ni Mukombozi wetu, na tunafanya yetu yote ili ‘kufuata hatua zake kwa ukaribu.’​—1 Petro 2:21; Luka 2:11.

 Uongo: Hamuamini kama Yesu alifufuliwa.

 Ukweli: Tunaamini kama Yesu alifufuliwa; tunajua kama ile njo musingi wa imani ya Kikristo na tunaikaziaka sana wakati tuko nahubiri.​—1 Wakorinto 15:3, 4, 12-15.

 Uongo: Hamuhangaikie kuona watoto wenu wanakosa ile furaha ya sherehe ya Pasaka.

 Ukweli: Tunapenda watoto wetu, na tunatumia wakati mingi juu ya kuwazoeza na kuwasaidia wakuwe na furaha.​—Tito 2:4.

Juu ya nini Mashahidi wa Yehova hawasherehekeake Pasaka?

  •   Sherehe ya Pasaka haitegemee Biblia.

  •   Yesu alitupatia amri ya kukumbuka kifo yake, hapana ufufuo wake. Tunafanyaka ile ukumbusho kila mwaka mu tarehe ya kifo yake kulingana na kalendari ya miezi ya Biblia .​—Luka 22:19, 20.

  •   Tunaamini kama mambo yenye watu wanafanyaka wakati wa kusherehekea Pasaka, inatokana na desturi zenye watu walikuwa wanafuata zamani juu wapate nguvu ya uzazi; kwa hiyo Mungu hapende watu wake wakuwe wanasherehekea Pasaka. Anapenda watu “washikamane na yeye tu,” na anachukia ibada yenye iko amo matendo yenye haimupendeze.​—Kutoka 20:5; 1 Wafalme 18:21.

 Tunaamini kama uamuzi wetu wa kukatala kusherehekea Pasaka unategemea kabisa Biblia, yenye inatutia moyo tukuwe na “hekima yenye kutenda na uwezo wa kufikiri” kuliko tu kufuata desturi za wanadamu. (Mezali 3:21; Matayo 15:3) Hata kama tunaambiaka watu wengine kuhusu imani yetu juu ya Pasaka, kama wanatuuliza, tunaheshimiaka haki ya kila mutu ya kujiamulia ikiwa ataisherehekea ao hapana.​—1 Petro 3:15.