Ona video zinazopatikana

Walisimama ili Kunisaidia

Walisimama ili Kunisaidia

 Siku moja yenye kulikuwa baridi na upepo mukali katika muji wa Alberta mu inchi ya Kanada, Bob alikuwa anatembeza gari yake kwa mwendo wa kilometre 100 kwa saa, kisha gurudumu (pneu) ya kushoto ya gari yake ikapasuka. Bob hakujua kama kulitokea nini, kwa hiyo, aliendelea kutembeza gari yake; kulikuwa kunabakia tu kilometre ingine tano ili afike kwake.

 Mu barua yenye alituma kwenye jumba la Ufalme la eneo lake, Bob alifasiria mambo yenye ilitokea kisha. Aliandika hivi: “Vijana tano wenye walikuwa ndani ya gari walikuja karibu na gari yangu na wakashusha dirisha la gari yao. Waliniambia kama gurudumu yangu ilikuwa imepasuka. Tulisimamisha gari zetu pembeni ya barabara, na wakajitolea kubadilisha ile gurudumu. Sikukuwa hata najua kama nilikuwa na gurudumu ingine ao kifaa cha kusaidia kuinua gari. Wakati nilikaa kwenye kiti changu cha vilema pembeni ya barabara, waliingia chini ya gari yangu na wakaona gurudumu ingine na pia kifaa cha kusaidia kuinua gari, na wakabadilisha ile gurudumu yenye ilipasuka. Kulikuwa baridi sana, na teluji (neige) ilikuwa inaanguka. Walikuwa wamevaa nguo za muzuri, lakini walifanya ile kazi na wakanisaidia niendelee na safari. Singeweza kufanya ile kazi mimi mwenyewe.

 “Ninashukuru sana wale vijana tano Mashahidi wenye walinisaidia. Walikuwa wanatembelea watu wa eneo hilo ili kuwahubiria. Kwa kweli, vijana hawa wanaishi kupatana na mambo yenye wanafundisha. Walinisaidia katika hali ngumu sana na yenye ingenipotezea wakati mingi, na niko mwenye shukrani sana kwa ajili ya ile. Kwa kweli, wale vijana walikuwa kama malaika wenye Mungu alinitumia ile siku.”