Hamia kwenye habari

APRILI 9, 2015
VANUATU

Mashahidi wa Yehova Watoa Msaada Baada ya Tufani ya Pam

Mashahidi wa Yehova Watoa Msaada Baada ya Tufani ya Pam

NOUMEA, New Caledonia—Usiku wa Machi 13, 2015, Tufani ya Kitropiki ya Pam ilipiga visiwa vya Pasifiki vya nchi ya Vanuatu kwa kasi ya upepo wa Daraja la 5. Ripoti za awali kutoka katika ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ya New Caledonia inaeleza kuwa hakuna Shahidi aliyekufa au kujeruhiwa nchini Vanuatu kwenye dhoruba hiyo kali. Kiasi cha uharibifu uliosababishwa na tufani hiyo bado unachunguzwa, lakini imethibitishwa kuwa katika kisiwa cha Efate, nyumba 31 za Mashahidi ziliharibiwa kabisa na 58 zinahitaji marekebisho. Katika kisiwa cha Tanna, karibu nyumba zote za Mashahidi ziliharibiwa na nyingine kuharibiwa kabisa. Tufani hiyo pia iliharibu Majumba matatu ya Ufalme, na lingine lilibomoka baada ya kuangukiwa na mti.

Halmashauri ya kutoa msaada katika mji mkuu wa Vanuatu, Port Vila, imetoa msaada wa chakula, maji safi, na makao ya muda kwa familia 100 hivi za Mashahidi. Pia, tani moja za msaada uliohitajika zilitumwa kwa Mashahidi waliopo Tanna. Ofisi ya tawi ya Australia inafanya kazi pamoja na ofisi ya tawi ya New Caledonia ili kutegemeza kazi ya kutoa msaada, ambayo inatia ndani kujenga makao ya muda, kurekebisha nyumba zilizoharibiwa, na kusambaza magodoro, nguo, na mahitaji mengine.

Jean-Pierre Francine, msemaji wa Mashahidi wa Yehova jijini New Caledonia, alisema hivi: “Tunathamini sana kwa msaada wa kutoka nga’mbo na wa kutoka kwa mashirika ya serikali uliowasaidia waamini wenzetu. Kwa kuwa safari za ndege kuja Vanuatu zimeanza tena, mwakilishi kutoka ofisi ya tawi ya New Caledonia na wahudumu wasafirio wanafanya ziara ili kutoa si msaada wa kimwili tu bali pia kutoa faraja na msaada wa kiroho.”

Wanahabari Wanaweza Kuwasiliana na:

J. R. Brown, Ofisi ya Habari za Umma, simu +1 718 560 5000

New Caledonia: Jean-Pierre Francine, simu +687 43 75 00