Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SWALI LA 7

Biblia Ilitabiri Nini Kuhusu Siku Zetu?

“Taifa litapigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme . . . Mambo hayo yote ni mwanzo wa maumivu ya taabu.”

Mathayo 24:​7, 8

“Manabii wengi wa uwongo watatokea na kuwapotosha wengi; na kwa sababu ya kuongezeka kwa uasi-sheria, upendo wa wengi utapoa.”

Mathayo 24:​11, 12

“Mtakaposikia kuhusu vita na habari za vita, msiogope; lazima mambo hayo yatukie, lakini ule mwisho bado.”

Marko 13:7

“Kutakuwa na matetemeko makubwa ya ardhi, na magonjwa na upungufu wa chakula katika sehemu mbalimbali; pia kutakuwa na mambo yenye kuogopesha na ishara kubwa kutoka mbinguni.”

Luka 21:⁠11

“Katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, wenye kujidai, wenye majivuno, wakufuru, wasiotii wazazi, wasio na shukrani, wasio washikamanifu, wasio na upendo wa asili, wasiotaka makubaliano yoyote, wachongezi, wasiojizuia, wakali, wasiopenda wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, waliojaa kiburi, wanaopenda raha badala ya kumpenda Mungu, wakionekana kama watu wanaomwogopa Mungu lakini wakizikana nguvu zake.”

2 Timotheo 3:​1-5