JE, NI KAZI YA UBUNI?
Mkia wa Mjusi Anayeitwa Agama
MJUSI anayeitwa agama huruka kutoka mahali tambarare hadi ukutani bila matatizo yoyote. Lakini iwapo mahali tambarare ni laini, mjusi huyo huteleza lakini bado anafaulu kuruka na kujishikilia ukutani. Anafanyaje hivyo? Siri ya mjusi huyo ni mkia wake.
Fikiria hili: Mijusi hao wanaporuka kutoka kwenye eneo tambarare lenye mikwaruzo
Mkia wa mjusi huyo unaweza kuwasaidia mainjinia kubuni magari ya roboti yasiyoanguka kwa urahisi ambayo yanaweza kutumiwa kuwatafuta waokokaji baada ya tetemeko la nchi au msiba mwingine. “Roboti hazina uwezo wa kujisawazisha kama wanyama,” anasema mtafiti Thomas Libby, “kwa hiyo, chochote kinachoweza kuzifanya ziwe imara zaidi ni maendeleo.”
Una maoni gani? Je, mkia wa mjusi anayeitwa agama ulijitokeza wenyewe? Au ulibuniwa?