Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jina la Mungu (lililowekewa alama) kama lilivyoandikwa katika hati za kale za Biblia

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Je, Mungu ana jina?

BAADHI YA WATU HUSEMA kwamba Mungu hana jina, wengine husema anaitwa Mungu au Bwana, na wengine husema Mungu ana majina mengi. Wewe una maoni gani?

BIBLIA INASEMA HIVI

“Wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”—Zaburi 83:18.

MAMBO MENGINE TUNAYOJIFUNZA KATIKA BIBLIA

  • Ingawa Mungu ana majina mengi ya cheo, amejipa jina moja tu.—Kutoka 3:15.

  • Mungu si fumbo; anataka tumjue. —Matendo 17:27.

  • Kujua jina la Mungu ni hatua ya kwanza ya kuwa rafiki yake.—Yakobo 4:8.

Je, ni kosa kutaja jina la Mungu?

UNGEJIBUJE SWALI HILO?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Labda

BIBLIA INASEMA HIVI

“Usilitumie jina la Yehova Mungu wako kwa njia isiyofaa.” (Kutoka 20:7) Ni vibaya kutumia jina la Mungu kwa njia inaonyesha kwamba huliheshimu.—Yeremia 29:9.

NI NINI KINGINE TUNACHOJIFUNZA KATIKA BIBLIA?